• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RAIS SAMIA ANAVYOWATUA NDOO KICHWANI WANANCHI WA RUVUMA

Imewekwa kuanzia tarehe: March 2nd, 2024

Na Albano Midelo

WANANCHI wa Mkoa wa Ruvuma wanaendelea kunufaika na  uongozi wa serikali ya Awamu ya Sita ambapo katika kipindi cha mwaka 2022/2023  serikali ilitenga bajeti ya  zaidi ya shilingi bilioni 28.7 kutekeleza miradi ya maji mkoani Ruvuma.

Meneja wa Wakala wa Maji Mijini na Vijijini (RUWASA)  Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Rebman Ganshonga anasema hadi sasa serikali imeleta zaidi ya shilingi bilioni 19  kutekeleza miradi hiyo  katika wilaya za Songea,Mbinga,Nyasa,Namtumbo na Tunduru.

Anasema katika kipindi cha mwaka 2023/2024 serikali  imetenga zaidi ya shilingi bilioni 26.2  kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji mkoani Ruvuma.

Anaitaja baadhi ya miradi iliyoidhinishiwa fedha wilayani Mbinga kuwa ni mradi wa maji  Linda milioni 450,mradi wa maji Tukuzi milioni 450,mradi wa maji Mtama milioni 400,mradi wa maji Kipololo milioni 400,mradi wa maji Kigonsera milioni 300 na mradi wa maji Ngima milioni 253.

Katika Wilaya ya Songea miradi iliyoidhinishiwa fedha anaitaja kuwa ni mradi wa maji Lwangeni milioni 618,mradi wa maji Lipaya bilioni 1.9,mradi wa maji Lipokela milioni 734.74,mradi wa maji Kizuka milioni 730.4,mradi wa maji Mtyangimbole bilioni 5.56 na mradi wa maji Ndelenyuma bilioni 1.6.

Meneja huyo wa maji Mkoa wa Ruvuma anaitaja  baadhi ya miradi ya maji  katika Wilaya ya Nyasa kuwa ni  ukarabati wa mradi wa maji Ng’ombo shilingi milioni 130,ukarabati wa mradi wa maji Lunyele milioni 280,mradi wa maji Mbuyula-Ndengele shilingi milioni 649.86 na mradi wa maji Mitomoni milioni 944.

Mhandisi Ganshonga anaitaja miradi ya maji iliyoidhinishiwa fedha katika kipindi cha mwaka 2023/2024 wilayani Namtumbo kuwa ni mradi wa maji Naikesi milioni 179.5,mradi wa maji Likusanguse milioni 300,mradi wa maji Mchomoro milioni 320.14 na mradi wa maji Msisima milioni 168.

Miradi ya maji katika wilaya ya Tunduru anaitaja kuwa ni  mradi wa maji Namwinyu milioni 535,mradi wa maji Hulia milioni 300,mradi wa maji Tuwemacho milioni 150,mradi wa maji Msinji milioni 200,Mradi wa maji Msechela milioni 200,mradi wa maji Nakapanya milioni 150 na mradi wa maji Masonya milioni 94.95.

“Utekelezaji wa miradi hiyo umeongeza huduma za upatikanaji wa maji kutoka asilimia 58.4 mwaka 2018 hadi kufikia asilimia 70 mwaka 2023,kuongeza  huduma ya maji kutoka watu 891,616 mwaka 2018 hadi kufikia watu 1,035,325 mwaka 2023’’,anasema Ganshonga.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas anasema  asilimia 70 ya watu wanaoishi vijijini mkoani Ruvuma ambao ni 1,294,156 kulingana na sensa ya watu ya mwaka 2022  wanapata huduma ya maji safi na  salama ambapo lengo la Mkoa  ni kufikia asilimia 85 kupata maji safi na salama kwa wakazi wa vijijini ifikapo mwaka 2025.

Kanali Thomas anabainisha kuwa Rais Dkt.Samia ameongeza idadi ya vijiji vyenye huduma ya maji  kufikia 366 kati ya vijiji 533 vilivyopo Mkoani Ruvuma.

Kanali Laban anasisitiza kuwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuwatua ndoo kichwani wananchi wa Mkoa wa Ruvuma na kwamba hadi kufikia Juni 30,2023 Mkoa wa Ruvuma ulikuwa unatekeleza jumla ya miradi 33 ya maji yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni zaidi ya bilioni 55.

Naye Mhandisi wa Maji Wilaya ya Songea Mhandisi Mathias Charles  anampongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa  shilingi bilioni 11.2 katika Wilaya hiyo ili  kutekeleza miradi sita ya maji  katika kipindi cha mwaka 2023/2024.

Stella Mhagama Mkazi wa  Kijiji cha Lipaya wilayani Songea  anamshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za kutekeleza mradi  wa maji  ambapo anasema kwa miaka mingi wanawake na Watoto wamekuwa wanapata kero ya kusafiri umbali mrefu kufuata maji mtoni na kubeba kichwani.

Diwani wa Kata ya Mpitimbi wilayani Songea Mheshimiwa Issa Kindamba  anampongeza Rais Dkt.Samia kwa kutoa fedha nyingi za kutekeleza mradi wa maji Lipaya ambao anasema unakwenda kupunguza umbali wa wananchi kutembea kufuata maji na kupunguza magonjwa yanayosambazwa na maji yasiyo salama.

Romanus Ndunguru Mkazi wa Kijiji cha Utili wilayani Mbinga anaishukuru serikali ya Awamu ya Sita  kwa kuwajengea mradi wa maji Utiri kwa gharama ya shilingi milioni 428  ambao  umekamilika kwa asilimia 99 na unakwenda kuhudumia watu 3,626.

Anania Nkomola Mkazi wa Kijiji ch Hinga wilayani Nyasa kwa niaba ya wananchi wenzake anamshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea mradi mkubwa wa maji Ngumbo wenye thamani ya shilingi bilioni 2.5 ambao tayari wananchi wameanza kunufaika nao.

Wananchi wa Kata ya Liuli wanamshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  kwa kutekeleza mradi wa maji katika Kijiji cha Hongi Kata ya Liuli wilayani Nyasa ambao umegharimu shilingi bilioni 4.7 ambapo hadi sasa mradi umeanza kuwahudumia wananchi.

Mrad mwingine mkubwa wa maji wilayani Nyasa ni ule ambao unatekelezwa katika kijiji cha Mwerampya kata ya Lituhi unaogharimu shilingi bilioni 6.5 ambapo tayari baadhi ya vijiji vimeanza kunufaika na mradi huo.

Nao wakazi wa Misechela wilayani Tunduru  akiwemo Amina Mohamed na Mariam Hussein wanaishukuru serikali kwa kuanza kutekeleza mradi mkubwa wa maji  ya bomba wenye thamani ya shilingi bilioni tatu ambapo wananchi hivi sasa wanapata huduma ya maji katika visima vinavyotumia pampu za mkono.

Hakuna ubishi wananchi wa Mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla moja ya vitu ambavyo watamkumbuka Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ni namna anavyoshughulikia kwa ufanisi wa hali ya juu changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa vijijini na mijini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.