• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC ABBAS aipongeza Manispaa ya Songea kwa kutekeleza maagizo ya Kamati ya LAAC

Imewekwa kuanzia tarehe: April 1st, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kutekeleza maagizo sita kati ya nane yaliyotolewa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC)  mwaka 2022.

Kanali Abbas  ametoa pongezi hizo wakati anazungumza kwenye kikao  cha kujadili utekelezaji wa maagizo ya Kamati ya  LAAC kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Hata hivyo amezitaja hoja za miaka ya nyuma  katika Halmashauri hiyo ambazo bado hazijafanyiwa kazi kikamilifu ili ziweze kufungwa ni 12 na kwamba kuna hoja na mapendekezo 53  ambayo yanatakiwa kufungwa na kufanyiwa kazi.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma pia ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo kutekeleza maagizo Matano kati ya sita ya Kamati ya LAAC.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea kati ya maagizo matatu yaliyotolewa na LAAC ni maagizo mawili yametekelezwa na kufungwa huku agizo moja utekelezaji wake haujakamilika kwa kipindi cha miaka minne sasa.

“Katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea jumla ya hoja na mapendekezo 44 bado hayajafanyiwa kazi ili yafungwe hivyo nawaomba waheshimiwa madiwani kufanya ufuatiliaji wa karibu ili kuhakikisha hoja zote zinajibiwa ipasavyo’’,alisisitiza RC Abbas.

Akizungumza kwa nyakati tofauti katika Halmashauri hizo,Mkuu wa Mkoa ameziagiza Halmashauri hizo kuhakikisha zinafanya maandalizi ya majibu ya hoja mapema na kwamba Halmashauri zichukue mapema hatua za kinidhamu kwa watumishi wanaozalisha hoja.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mheshimiwa Menas Komba ameahidi kuhakikisha hoja zote zilizosalia katika Halmashauri hiyo zinajibiwa na kufungwa sanjari na kusimamia kasi ya ukusanyaji wa mapato.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Mheshimiwa Michael Mbano,amesema  Halmashauri imejitahidi kutekeleza maagizo sita ya LAAC  na kwamba maagizo  mawili yaliyosalia itayatekeleza ili yaweze kufungwa.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amefanya vikao vya kujadili utekelezaji wa maagizo ya Kamati ya LAAC yaliyotolewa katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 katika Halmashauri za Nyasa,Mbinga Mji, Namtumbo,Halmashauri ya Willaya ya Songea,Manispaa ya Songea na  Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.