• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC IBUGE aagiza vituo vya kutolea huduma za afya vifungwe mifumo ya kukusanya mapato

Imewekwa kuanzia tarehe: June 11th, 2021


MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge  ametoa miezi mitatu kwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi kuhakikisha kuwa vituo vyote vya kutolea huduma za afya kwa umma vinafungwa mifumo ya kukusanya mapato (GOTHOMIS).

Brigedia Jenerali Ibuge ametoa agizo hilo wakati anafungua kikoa cha mfumo wa ugavi wa bidhaa za afya kwa viongozi wa serikali kutoka Halmashauri na wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma ambacho kimefanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Mkuu wa Mkoa ametoa agizo hilo kutokana na vituo vingi vya serikali kukosa mifumo ya kukusanya mapato (GOTHOMIS) ambapo takwimu zinaonesha kuwa kati ya vituo 280 vya kutolea huduma za afya vilivyopo mkoani Ruvuma,ni vituo kumi tu ndivyo vimefungwa mifumo hiyo.

“Kufikia Septemba Mosi,2021,vituo vyote vya kutolea huduma za afya kwa umma,viwe vimefungwa mifumo ya GOTHOMIS bila kukosa,Septemba 2,2021,niwe nimepata taarifa ya utekelezaji na baada ya hapo,ukaguzi wa kushitukiza utaendelea na kuchukua hatua’’,amesisitiza RC Ibuge.

Mkuu wa Mkoa pia amewaagiza wakuu wa Wilaya na wakurugenzi katika Halmashauri zote,kuhakikisha mapato na matumizi ya vyanzo vyote katika Halmashauri yanajadiliwa kwenye vikao vya kisheria na amekitaja moja ya kigezo kitakachotumika kuangalia ufanisi wa ukusanyaji mapato katika Mkoa wa Ruvuma katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 ni lazima kufikia zaidi ya asilimia 80 ya mapato ya vyanzo vya sekta ya afya.

RC Ibuge ameziagiza Halmashauri zote kuhakikisha vituo vya kutolea huduma za afya kwa umma vinatuma kila mwezi kwa wakati madai ya huduma iliyotolewa kwa wanachama wa Mfuko wa Afya Jamii ulioboreshwa(iCHF) na Mfuko waTaifa wa Bima ya Afya(NHIF).

Kutokana na asilimia ndogo ya wananchi waliojiunga na (iCHF) mkoani Ruvuma,RC Ibuge ameziagiza Halmashauri zote kufanya uhamasishaji mkubwa wa jamii kujiunga na mfuko huo ambapo hadi sasa Mkoa umeandikisha kaya zilizohai 11,820 sawa na asilimia 3.3 wakati lengo ni kufikia kaya 180,085 sawa na asilimia 50.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dr.Jairy Kanga ameahidi kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa,ikiwemo kuongeza ukusanyaji mapato kupitia mfumo wa GOTHOMIS  na kuongeza uhamasishaji kwa jamii kujiunga na (iCHF).

Dr.Kanga amesema mfuko wa iCHF mkoani Ruvuma ulianza kutekelezwa mwaka 2019,ambapo kitaifa Mkoa ulishika nafasi ya mwisho ambapo hivi sasa Mkoa umepanda hadi kufikia nafasi ya 11 kitaifa na kwamba kikao kazi hicho kitaongeza ufanisi na tija.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Juni 11,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.