• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC Ibuge aongoza sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: December 9th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ameongoza Sherehe za maadhimisho ya Miaka sitini ya Uhuru wa Tanzania Bara.

Sherehe za Maadhimisho hayo imefanyika katika  Viwanja vya Shule ya Muhuwesi Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma.

Ibuge amesema  Miaka 60 iliyopita Tanzania Bara ilikata minyororo  ya ukoloni Mwaka 1961  Mwasisi Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwaongoza wananchi wa Tanganyika katika kuupokea uhuru.

’’Siku hiyo aibu ya takribani Miaka 77 ya kutawaliwa na wageni kutoka Ulaya ilifikia Ukomo tumetawaliwa na Waingereza Miaka 43 (1918-1961) na kabla yao  miaka 34  (1884-1918) ya ukoloni wa Ujerumani’’.

Hata hivyo ibuge ameelezea mafanikio tangu kupata Uhuru Tanzania hadi kufikia sasa ikiwemo sekta ya Elimu hali ya Kielimu ilikuwa duni sana hivyo watu wengi walikuwa wanakabiliwa na ujinga.

Amesema Mwalimu Nyerere alitangaza ujinga kuwa moja ya maadui watatu ya nchi yetu pamoja na umaskini na maradhi,ilisababishwa na ufinyu wa kupata Elimu hasa kwa Waafrika ikisababishwa na Serikali ya Kikoloni.

’’Wakati tunapata Uhuru Mkoa ulikuwa na Shule za msingi 46 leo hii Mkoa una shule za msingi 818,shule za Sekondari zilikuwa 3 mpaka kufikia sasa Mkoa unashule za Sekondari 214, takwimu zinaonyesha mafanikio na kutufanya tutembee kifua mbele’’.

Akizungumzia upande wa Sekta ya Afya amesema mwaka 1961 Mkoa ulikuwa na Zahanati 8 na Hospitali 4 lakini mpaka kufikia sasa Mkoa wa Ruvuma una vituo 348 vinavyotoa huduma za Afya ikiwemo Zahanati 301 Vituo vya afya 34 na Hospitali 13.

Ibuge amezungumzia swala zima la Umeme  kabla ya Uhuru  mwaka 1961 hali ya upatikanaji wa Nishati ya Umeme ilikuwa Duni kwani isipokuwa baadhi ya maeneo machache,kwa sasa Mkoa umeunganishwa Umeme wa gridi ya Taifa katika Wilaya zote ikiwemo vijiji 319  vimepata na vijiji 235 vipo kwenye mpango.

Amesema sekta ya Miundombinu kabla ya  Uhuru ulipopatikana Mkoa wa Ruvuma haukuwa na Mtandao wa Barabara za kiwango cha lami kwa sasa Barabara  zina kiwango cha lami kilomita 700 za Barabara  za kiwango cha lami ambapo Wilaya zote 5 zimeunganishwa katika kiwango cha lami.

  Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Desemba 9,2021.                   

                                                                    

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.