• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC IBUGE azindua soko la ununuzi wa mahindi Mkoa wa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: August 16th, 2021

Mkoa wa Ruvuma una ziada ya mahindi tani 326,497

MKOA wa Ruvuma katika kipindi cha mwaka 2020/2021 umezalisha ziada ya mahindi tani 326,497 kati ya tani za mahindi 816,242 zilizozalishwa.

Akizungumza wakati anazindua soko la ununuzi wa zao la mahindi Kanda ya Songea mkoani Ruvuma katika kijiji cha Mgazini Halmashauri ya Songea,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amesema katika kipindi cha mwaka 2020/2021,wakulima wa mahindi wameweza kulima jumla ya hekta 276,488.

TAZAMA VIDEO YA UZINDUZI WA SOKO LA MAHINDI HAPA https://www.youtube.com/watch?v=j0jzllfFG0E&t=186s

"Uzalishaji huu ni zaidi ya kiwango kilichozalishwa kwa ongezeko la asilimia nne,ukilinganisha na kiwango cha uzalishaji katika msimu wa mwaka 2019/2020 ambapo tani 787,321 pekee zilizalishwa’’,alisisitiza Ibuge.

Brigedia Jenerali Ibuge amesema Mkoa una uwezo wa kuuza ziada hiyo ya mahindi ndani na nje ya nchi ambapo amewapongeza Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula NFRA kwa uamuzi wa kununua mahindi ambayo ni sehemu ya ziada.

Amesema katika awamu ya kwanza ya ununuzi kutakuwa na vituo tisa  katika Mkoa wa mzima ambavyo vimepangwa kwa lengo la kumrahisishia mkulima kuweza kununua mahindi yake bila kutumia gharama kubwa.

Hata hivyo amesema kiwango cha kununua tani 32,000 tu za mahindi kwa Mkoa wa Ruvuma ambacho kimewekwa na NFRA ni kidogo ukilinganisha na uzalishaji mkubwa wa mahindi uliofanywa na wakulima msimu huu.

Amesema mgawo huo ni kidogo hivyo ametoa rai kwa Wizara ya Kilimo  kupitia NFRA kuendelea kushirikiana kupanua wigo wa masoko ili wakulima wa Ruvuma waendelee kuzalisha ziada.

Ametoa rai kwa wanunuzi wengine nchini kote  kufika mkoani Ruvuma kuendelea kununua mahindi ili kuipunguza ziada iende kwa wengine nje ya nchi na maeneo mengine yenye uhaba wa chakula ambapo amewaomba kununua kwa bei nzuri ili kuleta tija kwa wakulima na kuwawezesha kulima kwa tija zaidi.

Awali Meneja wa NFRA Kanda ya Songea Ramadhani Nondo  alisema  kwa ujumla NFRA katika msimu wa mwaka 2020/2021,wanatarajia kununua tani za mahindi 165,000 ambapo  Kanda ya Songea imetengewa kununua mahindi tani 32,000 na kwamba kwa awamu ya kwanza zinanunuliwa tani 6,000 za mahindi.

Amesema mahindi yatanunuliwa kwa shilingi 500 kwa kilo katika kituo cha NFRA Ruhuwiko na vituo vingine mahindi yatanunuliwa kwa kilo shilingi 470 na kwamba ununuzi utafanyika kwenye vituo tisa vilivyopangwa ambavyo amevitaja kuwa ni Namtumbo mjini, Namabengo,Mgazini,Magagura,Mpitimbi,Mbinga mjini,Kigonsera na Ofisi za Kanda za NFRA Ruhuwiko.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Odo Mwisho ameiomba serikali iongeze kiwango cha tani za ununuzi  kwa sababu wananchi watauza kiasi kidogo cha mahindi ukilinganisha na uzalishaji,hivyo ameshauri  serikali inunue mahindi kupitia mfuko mkuu wa serikali ili yakauzwe kwenye mahitaji ya chakula ndani na nje ya nchi.

Amesisitiza kuwa wananchi wasipotafutiwe masoko ya uhakika ya mazao yao,wataendelea kupata hasara kwa kuuza kwa bei ndogo hali ambayo itawakatisha tamaa kuendelea kulima zao la mahindi.

Mkoa wa Ruvuma kwa mwaka wa tatu mfululizo umeendelea kushika nafasi ya kwanza kitaifa kwa kuongoza kwa uzalishaji wa mazao ya chakula.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Agosti 16,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.