• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA asikitishwa na hali ya malezi na uangalizi wa watoto

Imewekwa kuanzia tarehe: May 15th, 2024

Na Albano Midelo,Namtumbo

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed amesikitishwa na hali isiyoridhisha ya malezi na uangalizi wa mtoto.

Akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya familia ambayo kimkoa yamefanyika Kijiji cha Suluti wilayani Namtumbo,amesema wazazi na walezi wengi wamekuwa  hawatimizi ipasavyo majukumu ya malezi  na kusababisha malezi ya upande mmoja.

“Takwimu  kutoka ofisi ya Ustawi wa Jamii Mkoa kwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Desemba 2023 zinaonesha kuwa jumla ya mashauri 3,441 yalipokelewa na kushughulikiwa ambapo mashauri 1,611 sawa na asilimia 47 yalihusu matunzo ya watoto,mashauri 831 sawa na asilimia 24 yalihusu matatizo ya ndoa na mashauri 969 sawa na asilimia 29 yalihusu mashauri nje ya ndoa’’,alisema Kanali Abbas.

Amebainisha kuwa Ofisi ya Ustawi wa Jamii imekuwa ikipokea kesi za matunzo ya Watoto na malalamiko yanayoelekezwa upande wa akinababa.

Ametoa rai kwa wazazi na walezi ambao wamefarakana kutambua kuwa mtoto bado anastahili malezi yaliyo bora hivyo ni vema kuweka mpango mzuri wa kumlea mtoto ili asiathirike kimalezi na kwamba wazazi wajitahidi kuvumiliana ili kuepusha kuachana kusiko kwa lazima hivyo kumuathiri mtoto.

Akisoma risala ya maadhimisho ya siku ya kimataifa ya familia Mariam Juma ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ameitaja kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu inayosema tukubali tofauti zetu kwenye familia,kuimarisha malezi ya Watoto, inawakumbusha wazazi na walezi kuweka kando tofauti zao na kuangalia malezi na huduma zinazostahili kwenye familia.

Juma amebainisha kuwa katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Desemba 2023 mashauri 2,859 ya ukatili yalitolewa taarifa na kushughulikiwa katika ofisi  za ustawi wa Jamii Mkoa wa Ruvuma na kwamba mashauri 121 yalifikishwa mahakamani.

Hata hivyo amesema mashauri 77  sawa na asilimia 63.6 yalihukumiwa,kati ya mashauri 1,580 ya Watoto,mashauri 1050 sawa na asilimia 66.6 yaliwahusu wasichana wakati mashauri 1,279 ya watu wazima,mashauri 1,030 sawa asilimia 80.5 yaliwahusu wanawake.

Naye Mkuu wa Wilaya ya  Namtumbo Mheshimiwa Ngollo Malenya amesema wazazi wote wawili wanatakiwa kuwajibika kwa malezi ya familia ili fahari ya mtoto na mafanikio yake yawe kwa wazazi wote wawili kwa kuwa mtoto ni wa wazazi wote.

Amewashauri wazazi na walezi kuwalea Watoto kwa misingi inayompendekeza Mwenyezi Mungu na kuheshimu sheria za nchi,

Hata hivyo Malenya amesisitiza upendo kwa familia ambao unafanikisha malezi bora kwa familia na kutahadharisha kuwa wazazi na walezi wasipoungana kwa dhamira hawataweza kutimiza ndoto za Watoto wao.

Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa Mei 20,1993 lilitenga siku maalum ya maadhimisho ya siku ya kimataifa ya familia lengo likiwa ni kutambua nafasi ya familia katika jamii.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.