• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA azindua kituo cha mabasi Lundusi Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: July 1st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amezindua rasmi kituo cha mabasi cha Lundusi kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mradi uliotekelezwa kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) awamu ya pili kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji cha Lundusi.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Kanali Ahmed ameeleza kuwa TASAF ni nyenzo muhimu ya kupambana na umaskini kwa kuwa inawawezesha wananchi kutumia fursa za kuinua hali zao za kiuchumi.

“Awamu ya pili ya utekelezaji wa mpango wa TASAF umejikita sana katika masuala ya kuwezesha kaya kutumia fursa za kukuza uchumi na kuongeza kipato katika kaya za walengwa, kuboresha upatikanaji wa huduma za afya, elimu, maji safi na salama pamoja na miundombinu ya kukuza uchumi katika ngazi ya jamii,” alisema Kanali Ahmed.

Ameeleza kuwa ujenzi wa kituo cha mabasi pamoja na maduka ya biashara katika eneo hilo ni hatua muhimu ya kuimarisha uchumi wa kaya na jamii kwa ujumla, hivyo ametoa wito kwa viongozi na wananchi kuitunza miundombinu hiyo ili iendelee kutoa manufaa kwa wananchi na kuchangia maendeleo ya halmashauri.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bwana Shedrack Mziray, amesema TASAF ilitoa shilingi milioni 686.3 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa kituo hicho cha mabasi baada ya kupokea maombi kupitia halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Amesema kuwa tangu kuanzishwa kwa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini mwaka 2001, TASAF imekuwa ikitoa ruzuku kwa halmashauri zote nchini kwa lengo la kuwawezesha walengwa, na hadi kufikia sasa, jumla ya shilingi trilioni 1.17 zimetolewa na kuwafikia walengwa.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi. Mary Makondo, amesema kuwa mkoa utaendelea kushirikiana kwa karibu na TASAF ili kuhakikisha miradi iliyobaki inakamilika kwa wakati, huku wakiendelea kuratibu na kusimamia kwa ufanisi utekelezaji wa huduma za miradi ya maendeleo ili kuhakikisha wananchi wananufaika ipasavyo na uwekezaji huo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI yaanza kutekeleza mradi wa kituo cha afya Mbaha

    July 01, 2025
  • RC RUVUMA azindua kituo cha mabasi Lundusi Songea

    July 01, 2025
  • MTO Ruvuma mboni ya uhai na maajabu ya utalii kuisni mwa Tanzania

    June 30, 2025
  • SERIKALI yatoa bilioni 3.4 kumaliza kero ya maji Tunduru

    June 29, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.