• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC THOMAS atoa wito kwa GST kusogeza huduma za mahabara Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: September 22nd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanal Laban Thomas ametoa wito kwa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kufungua tawi katika maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa Makaa ya Mawe ikiwemo Mkoa wa Ruvuma. 

Kanal Thomas ameyasema hayo Ofisini kwake wakati akipokea toleo la Vitabu vipya vinavyoonesha Madini yapatikanayo Tanzania vya Mwaka 2023 vilivyoandaliwa na GST.

Amesema uzalishaji wa Makaa ya Mawe unafanyika kwa kiwango kikubwa mkoani humo ambapo wafanyabiashara wanatumia mianya ya kuto kuwa na maabara ya kutambua ubora wa Makaa hayo kupunguza bei ya bidhaa hiyo, hivyo ameiomba GST kusogeza huduma hiyo ili kuwapunguzia adha ya kusafirisha sampuli kupeleka nje ya nchi kwa ajili ya vipimo.

Aidha, amesema ameuongoza Mkoa huo kwa muda mrefu na hakuwahi kujua kuwa Mkoa huo una Madini mengi mbali na yale waliyozoea kuona yanavunwa ambapo ameahidi kusambaza taarifa za Madini yapatikanayo Mkoani humo kwa wadau mbalimbali pamoja na kuhuisha taarifa za madini kwenye website ya Mkoa  kwa lengo la kutafuta Wawekezaji.

Kwa upande wake, Meneja wa Sehemu ya Jiolojia Solomon Maswi amesema, jukumu kubwa la GST ni kufanya tafiti za madini, kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusiana na madini na kuratibu majanga ya asili ya jiolojia.

"Leo tumekuja ofisini kwako mahususi kukukabidhi Vitabu vya Madini yapatikanayo Tanzania ili uweze kujua rasilimali zilizopo mkoani kwako ambalo ni agizo la Waziri Mkuu ili kuvutia uwekezaji mkubwa katika eneo lako," amesema Maswi.

Pamoja na Mambo mengine, Maswi amesema Mkoa wa Ruvuma una madini mbalimbali tofauti na wadau wajuavyo kuwa ni Makaa ya mawe, urani na vito pekee, hivyo Kitabu hicho kinaonesha Madini hayo katika ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata mpaka Kijiji na hivyo kitasaidia kwa kiwango kikubwa kuhamasisha Wawekezaji kuja kufanya utafiti wa kina.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.