• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUVUMA kuimarisha uzalishaji wa zao la kahawa na parachichi

Imewekwa kuanzia tarehe: March 30th, 2025

Katika juhudi za kuboresha sekta ya kilimo na kuongeza kipato kwa wakulima, Mkoa umejipanga kuongeza uzalishaji wa mazao ya parachichi na kahawa kwa kiwango kikubwa ifikapo mwaka 2025.

Afisa Kilimo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Onesmo Ngao anaitaja Mikakati hii inalenga kuleta mageuzi makubwa kwenye sekta ya kilimo huku ikihamasisha wakulima kushiriki kikamilifu katika uzalishaji wa mazao haya yenye thamani kubwa sokoni.

Mapinduzi Katika Kilimo cha Parachichi

Kwa sasa, Mkoa unazalisha tani 1,768 za parachichi, lakini lengo ni kufikia tani 37,500 ifikapo mwaka 2025. Ili kufanikisha azma hii, Mkoa umeanzisha mkakati wa kuhamasisha wakulima kupitia vikundi mbalimbali vya kilimo.

Hadi sasa, juhudi hizo zimezaa matunda kwani tayari ekari 600 za parachichi zimekwishapandwa.

Mikakati hii inatekelezwa kwa kushirikiana na Taasisi ya SAGCOT (Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania), ambayo inaunga mkono jitihada za wakulima kwa kuwapatia elimu ya kilimo bora, mbegu zenye ubora wa hali ya juu, na kuwaunganisha na masoko ya parachichi ndani na nje ya nchi.

Wakulima wanaendelea kufaidika na mwelekeo huu mpya wa kilimo cha kibiashara, ambao unawapa fursa ya kupata kipato endelevu.

Kahawa Yapewa Kipaumbele

Sanjari na juhudi za kuinua kilimo cha parachichi,Ngao anabainisha kuwa  Mkoa wa Ruvuma pia umeweka malengo makubwa katika kilimo cha kahawa.

Kwa sasa, Mkoa unazalisha tani 23,355 za kahawa safi, lakini matarajio ni kufanikisha uzalishaji wa tani 55,000 ifikapo mwaka 2025.

Kwa msimu huu, masoko ya kahawa yanaendelea kushamiri, huku vyama vya msingi vikiendelea kukusanya kahawa kutoka kwa wakulima.

 Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo imekuwa ikihamasisha matumizi ya mbinu bora za kilimo cha kahawa ili kuongeza uzalishaji na ubora wa zao hili muhimu.

Mikakati hii ya Mkoa inaashiria mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo, ambayo yatawanufaisha wakulima kwa kuongeza kipato chao na kuinua uchumi wa eneo husika.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.