• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUVUMA kuendelea kununua soya na ufuta kupitia Mfumo wa Stakabadhi ghalani

Imewekwa kuanzia tarehe: June 26th, 2021

WADAU wa kilimo na Ushirika kutoka wilaya zote mkoani Ruvuma wamekubaliana kuwa hakuna soya wala ufuta utakaonunuliwa  na kutoka nje ya Mkoa wa Ruvuma bila kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani.

Wamepitisha azimio hilo katika mkutano wa uendeshaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani uliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge na kufanyika Ikulu Ndogo mjini Songea.

Mkutano huo umewashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wakuu wa wilaya,makatibu tawala,wakurugenzi wa Halmashauri, wenyeviti wa Halmashauri,Mstahiki Meya,viongozi wa vyama vikuu vya ushirika vya SONAMCU na TAMCU,Mwakilishi kutoka Bodi ya Leseni ya stakabadhi ghalani,maafisa kilimo na watumishi wengine.

“Tumekubaliana wote kwenye kikao hiki,hivyo mkasimamie,hakuna soya wala ufuta utakaonunuliwa kutoka nje ya Mkoa bila kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani’’,amesisitiza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.

RC Ibuge ameziagiza Halmashauri na wilaya zote mkoani Ruvuma kusimamia kikamilifu utekelezaji huo na kuongeza kuwa Halmashauri zina jukumu la kuunda na kuhuisha  Kamati za usimamizi wa stakabadhi ghalani ili kutatua changamoto ndogo ndogo za wadau.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma pia ameagiza elimu endelevu kuhusu   taratibu,sheria na miongozo iliyopo  katika mfumo wa stakabadhi ghalani ianze kutolewa kila Halmashauri na kwamba vyama vya ushirika vinahusika zaidi ili wadau wapate uelewe wa kina kuhusu umuhimu wa mfumo huo.

Mfumo wa stakabadhi ghalani  katika mazao ya soya na ufuta mkoani Ruvuma,umekuwa msaada katika kuwapatia wakulima kipato kikubwa ambapo takwimu zinaonesha kuwa  msimu wa mwaka 2018/2019 kiasi cha tani 2,855.38 za soya na tani 8,428.27 za ufuta ziliuzwa kupitia mfumo huo na kwamba mwaka 2019/2020 tani 1,499.8 za soya na tani 12,234.76 za ufuta ziliuzwa.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amemwagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Stephen Ndaki kuwasimamisha kazi watumishi watatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea na Manispaa ya Songea  wanaodaiwa kufanya udanganyifu kuwa sehemu ya ubadhirifu wa kuandika stakabadhi, kuingiza kwenye mfumo wa mapato na kibali.

RC Ibuge amewataja watumishi hao kuwa ni Noel Chengula,Mbaya Kitete na Hamisi Mwanaupanga ambapo Mkuu wa Mkoa  amemwagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma kuwasimamisha kazi ili wapishe taratibu za kisheria.

Mkuu wa Mkoa pia amemwagiza Mkuu wa TAKUKURU kufanya uchunguzi wa haraka ili suala hilo likamilike kisheria,huku akimwagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma kufanya ukaguzi katika mfumo wa mapato katika Mkoa na kuwasilisha taarifa kwake Julai 30 mwaka huu.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma pia amewaagiza wakuu wa Wilaya  na Kamati za Usalama kufanya kazi ya kufuatilia upotevu wa mapato ya ndani  katika Halmashauri zao na kupeleka taarifa kwake Juni 30 mwaka huu.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amewapongeza wafanyabiashara wa mazao mkoani Ruvuma kupitia chama chao cha Umoja wa Wanunuzi wa Mazao Vijijini Mkoa wa Ruvuma (UWAMAVIRU) kuwafichua watumishi wasio kuwa waaminifu na ambao wanatumia vituo vya ukaguzi wa mazao kwa maslahi yao binafsi.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Juni 26,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.