• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUVUMA waadhimisha kuzaliwa kwa Rais Dkt Samia kwa kupanda miti

Imewekwa kuanzia tarehe: January 27th, 2023

RUVUMA WAADHIMISHA KUZALIWA KWA RAIS SAMIA KWA KUPANDA MITI

Mkuu wa  Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amewaongoza wananchi  kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kupanda miti katika shule za Msingi  na sekondari Mashujaa Manispaa ya Songea.

Akizungumza mara baada ya kukamilisha zoezi hilo,Kanali Laban amesema Mkoa umeamua kuifanya shughuli  ya kupanda miti ya matunda ikiwa ni maalum kuunga mkono siku ya kuzaliwa kwa Rais.

“Nichukue fursa hii kumtakia heri na afya tele Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa,kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Ruvuma tunampongeza sana,Mwenyezi Mungu aendelee kumlinda ili aendelea kuliongoza Taifa letu la Tanzania’’,alisema

Amesema mara nyingi Rais Dkt.Samia amekuwa wanahimiza watanzania kupanda miti ya matunda hivyo katika tukio hilo ,Kanali Thomas ameongoza kupanda miti ya matunda aina ya miparachichi na mipera katika shule za msingi Mashujaa na shule ya sekondari Mashujaa.

“Jambo muhimu sio tu kupanda miti,bali kuhifadhi na kuilinda ili miti hiyo iweze kukua,miti hii kwa kuwa ni ya matunda inaweza kutumika kama chakula kwa wanafunzi hivyo kujenga afya za wanafunzi na wal’mu’’,alisema RC Thomas.

Mkuu wa Mkoa amewahimiza wananchi wote mkoani Ruvuma kuendelea kupanda miti nyumbani na kwenye mashamba ambapo amesema mashamba mengi ya kahawa hivi sasa yamebakia vipara baada ya miti kukatwa hivyo amewashauri wakulima kuhakikisha mashamba yao yanapandwa miti.

Amesema uzinduzi wa Kampeni ya wiki ya upandaji miti kimkoa  ilifanyika Januari Mosi mwaka huu ambapo jumla ya miti milioni 1.1 ilipandwa ambapo amesema zoezi la upandaji miti ni endelevu hadi mvua zitakapoishia.

Afisa Maliasili Mkoa wa Ruvuma Africanus amesema kwenye zoezi hilo maalum lililoongozwa na Mkuu wa Mkoa jumla ya miti 400 imepandwa kati ya hiyo miti ya matunda 200 na miti ya kupanda kwenye mipaka 200.

Mkoa wa Ruvuma  kwa mwaka 2023 unatarajia kupanda miti ya aina mbalimbali zaidi ya milioni nane ambayo inapandwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS), Taasisi za Serikali, Taasisi binafsi na wananchi.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Januari 27,2023

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.