• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUWASA Namtumbo ilivyodhamiria kusogeza huduma ya maji jirani ya wananchi

Imewekwa kuanzia tarehe: March 17th, 2022

WIZARA ya maji kupitia wakala wa maji safi na usafi wa mazingira vijijini(Ruwasa)wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma,imeanza kutekeleza miradi ya maji katika vijiji mbalimbali ambavyo kwa muda mrefu havikuwa na huduma hiyo.
Kaimu Meneja wa Ruwasa wilaya ya Namtumbo Salum Nachundu, alitaja miradi hiyo ni pamoja na mradi wa maji Mkongo Gulioni-Nahimba uliotekelezwa chini ya Programu ya maendeleo ya sekta ya maji(WSDP)kupitia program ndogo ya maji na usafi wa mazingira vijijini(RWSSP).

Alisema, mradi huo ulianza kutekelezwa mwaka 2017na mkandarasi Kipera Contractors ambaye alitakiwa kukamilika kazi mwaka 2020,lakini alishindwa kukamilisha kazi kutokana na changamoto mbalimbali ikiwamo uwezo mdogo wa kiufundi na fedha.
Nachundu alieleza kuwa,baada ya Serikali kukatisha mkataba na mkandarasi, mradi huo umekamilishwa na wakala wa maji safi na usafi wa mazingira vijijini(Ruwasa) kwa njia ya force akaunti ambapo kwa sasa umekamilika na wananchi wanapata huduma.
Kwa mujibu wa Nachundu,mradi wa Mkongo gulioni-Nahimba ulisanifiwa kuhudumia wakazi 8,007 katika vijiji hivyo ambapo awali gharama ya mradi ilikuwa Sh.2,069,975,521,hata hivyo zilipungua hadi Sh.1,451,531,411 baada ya Ruwasa kutekeleza mradi huo kwa kuwatumia mafundi wa kawaida.
Aidha, alitaja mradi mwingine unaotekelezwa ni katika kijiji cha Masuguru ambao unatarajia kuhudumia wananchi wapatao 3,264 na gharama za mradi huo ni Sh.402,000,000.
Kwa upande wake msimamizi wa mradi huo Gloria Nziku alisema,mradi wa maji katika kijiji cha Msuguru unatekelezwa chini ya program ya malipo kwa matokeo na ulianza kutekelezwa mwezi Agosti mwaka 2021 na unatarajia kukamilika tarehe 30 mwezi huu.Nziku,ameishukuru wizara ya maji kutoa fedha na serikali ya kijiji na wananchi,kwa ushirikiano mkubwa waliotoa wakati wa utekelezaji wa mradi huo ambao hadi sasa umefikia asilimia 85.Alisema,mradi utakapokamilika jumuiya ya watumia maji Masuguru ndiyo watakuwa wasimamizi wakuu na waendeshaji wa mradi huo.
Amewataka viongozi wa jumuiya na wananchi kuhakikisha wanalinda miundombinu ya mradi ili uendelea kufanya kazi kama ilivyokusudiwa na serikali.
Mkazi wa kijiji hicho Dolfina Chowo alisema,wanachangamoto kubwa yam aji safi na salama ambapo wanatumia maji ya visima vya kupampu na wakati mwingine maji ya visima na mito iliyopo kando ya kijiji hicho.
Alisema, sasa wana matumaini makubwa ya kuondokana na kero hiyo baada ya serikali kupitia wakala wa maji safi na usafi wa mazingira(Ruwasa)kuanza kutekeleza mradi wa maji ya bomba ambao umeanza kuleta matumaini makubwa kwao.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.