• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SEKONDARI ya wasichana ya Dkt.Samia Suluhu Hassan yaanza kuchukua wanafunzi

Imewekwa kuanzia tarehe: September 1st, 2023

SEKONDARI ya wasichana ya Dkt.Samia Suluhu Hassan iliyojengwa katika kata ya Rwinga wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma kwa gharama ya shilingi bilioni nne imeanza kuchukua wanafunzi wa kidato cha tano.

Mkuu wa Shule hiyo Mwl.Dafrosa Chilumba amesema ili kutekeleza mradi wa ujenzi wa sekondari hiyo serikali ya Awamu ya Sita  inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  katika awamu ya kwanza ilitoa shilingi bilioni tatu.

Ameyataja majengo ambayo yalijengwa katika awamu ya kwanza  ya ujenzi ulianza Aprili 2022 kuwa ni ujenzi wa jengo moja la utawala,madarasa 12 na maabara nne za Jiografia,Kemia,Fizikia na Biolojia.

Majengo mengine ameyataja kuwa ni nyumba mbili za walimu zenye uwezo wa kuchukua  familia tatu,mabweni Matano yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 120 kila bweni,mfumo wa maji safi wenye matanki mawili na mitaro yenye urefu wa mita 1050,vyoo matundu 16,bwalo kubwa la chakula,chumba cha jenereta,njia za kutembea  na uzio.

Hata hivyo amesema utekelezaji wa ujenzi katika awamu ya kwanza umefikia zaidi ya asilimia 95 na kwamba serikali imeleta shilingi bilioni 1.1 kuanza kutekeleza mradi kwa awamu ya pili.

Ameitaja miundombinu ambayo inajengwa katika awamu ya pili kuwa ni ujenzi wa madarasa kumi,nyumba mbili za walimu zenye uwezo wa kuchukua familia nne,jengo la TEHAMA, maktaba,mabweni manne yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 80 kila moja.

“Wanafunzi wa kidato cha tano ambao tumepangiwa na serikali kuanza masomo ni 249  wengi wameshafika,wanafunzi hao wanasoma michepuo mitano ,wanafunzi wanafurahia mazingira ya kuvutia yenye huduma zote muhimu,walimu wapo wa kutosha,hakuna mwanafunzi anayewaza kuhama’’,alisisitiza.

Stella Magaho ni Mwanafunzi wa Kidato cha Tano katika sekondari ya Wasichana ya Dkt.Samia Suluhu Hassan  mchepuo wa PCB  amesema wanafunzi walioripoti katika shule hiyo wanafurahia mazingira rafiki ya kusoma na kwamba hakuna changamoto yoyote .

Mwanafunzi huyo ambaye ni Kiranja Mkuu kwa niaba ya wenzake anaishukuru serikali kwa kuwajengea sekondari bora kwa Watoto wa kike ambapo ameahidi watafanya vizuri katika masomo yao.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema sekondari ya wasichana ya Namtumbo ni miongoni wa sekondari mpya 11 ambazo Rais Dkt.Samia ametoa zaidi ya shilingi bilioni 7.7. kujenga sekondari hizo mkoani Ruvuma katika mwaka wa fedha 2022/2023.

Kanali Thomas  amezitaja shule hizo mpya kuwa  zimejengwa katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma na kwamba shule zimejengwa kupitia mradi wa kuboresha Elimu ya Sekondari nchini (SEQUIP).

Hata hivyo amesema katika Halmashauri ya Tunduru zimejengwa shule tatu za sekondari kupitia mradi wa SEQUIP na kwamba katika Halmashari ya Namtumbo pia zimejengwa shule mbili ikiwemo shule ya wasichana ya Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mheshimiwa Deogratias Ndejembi amesema serikali ya Awamu ya sita katika mwaka 2022/2023 imetoa zaidi ya shilingi bilioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya za sekondari 176 za kata kupitia program ya SEUIP.

“Fedha hizo zimetolewa kujenga shule za sekondari za kata katika kata zisizo na shule na kata zenye wanafunzi wengi zaidi ukilinganisha na miundombinu ya shule zilizopo’’,alisisitiza Ndejembi.

Hata hivyo amesema katika Mkoa wa Ruvuma kupitia program hiyo mwaka huu,serikali imetoa shilingi bilioni 3.9 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya saba za sekondari za kata.

Sekondari ya wasichana ya Dkt.Samia Suluhu Hassan iliyopo Namtumbo mkoani Ruvuma ni miongoni mwa sekondari kumi  mpya za wasichana za mikoa  zilizojengwa na serikali ya Awamu ya Sita.

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.