• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERA ya elimu ya mwaka 2014 inavyowanufaisha watoto wa kike

Imewekwa kuanzia tarehe: February 20th, 2020

SERA ya elimu ya mwaka 2014 imepata mafanikio makubwa kwa watoto wa kike baada ya mahudhurio ya wanafunzi wa kike kufikia asilimia 52 huku watoto wa kiume ikifikia asilimia 48.

Akizungumza katika kongamano la wanawake Kanda ya kusini lilofanyika mjini Songea, kuelekea maadhimisho ya siku wanawake duniani,Mwakilishi wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Hanifa Selengu amesema sera hiyo imetekelezwa na serikali ya Awamu ya tano kwa mafanikio makubwa.

Selengu amesema serikali imetenga kila mwezi kiasi cha shilingi bilioni 25 ili kuhakikisha kuwa kila mtoto mwenye haki ya kupata elimu anakwenda shule hali ambayo imesababisha uandikishaji wa wanafunzi katika shule za msingi na sekondari kuongezeka zaidi ya mara tatu.

“Wanataaluma wanasema watoto wa kike wanapoongezeka katika kupata elimu,uchumi wa     nchi pia unaongezeka’’,alisema Selengu.

Kulingana na Mwakilishi huyo wa Wizara ya Afya,utekelezaji wa sera hiyo umezipa pengo la mahudhurio sawa ya elimu  kwa watoto wa kike na kiume ambapo takwimu za BEST za mwaka 2018 zinaonesha kuwa katika shule za serikali wanafunzi wanaokwenda shule ni asilimia 6.9.

Hata hivyo amesema kitendo cha serikali kuondoa ada katika shule za serikali kumesababisha kuongezeka kwa wanafunzi katika shule za msingi kutoka 9.317,791 mwaka 2017 hadi kufikia  wanafunzi 10,111,671 mwaka 2018.

Akizungumza kabla ya ufunguzi wa kongamano hilo mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isabela Chilumba amelitaja lengo la kongamano hilo kuwa ni kujadili kwa pamoja hali ya elimu katika kanda ya Kusini na umuhimu katika kuleta maendeleo endelevu.

Mndeme amesema kongamano hilo pia litajadili fursa za uongozi kwa wanawake na hali ya ukatili wa kijinsia katika jamii na kupanga mkakati wa kufikia maendeleo ya jamii endelevu.

Amesema serikali imechukua hatua mbalimbali za kukabiliana na ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto kuhakikisha unatokomezwa pamoja na kuwawezesha wanawake kiuchumi.

“Mpango wa Taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto unatekelezwa kwa lengo la kupunguza ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2022’’,alisisitiza.

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo kitaifa ambayo yanafanyika Machi 8 mwaka huu mkoani Simuyi ni “Kizazi cha usawa kwa maendeleo ya Tanzania sasa nay a baadaye’’.

Katika kongamano hilo wanawake wamelitumia kuonesha bidhaa mbalimbali  wanazotengeza na kuzalisha katika Mkoa wa Ruvuma.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Februari 19,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.