• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI kutoa maamuzi ya soko la madini ya vito Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: May 16th, 2024

Na Albano Midelo

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed amesema ndani ya siku saba kuanzia Mei 15,2024,serikali itatoa maamuzi ya uwepo wa soko moja au masoko matatu ya madini ya vito wilayani Tunduru.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake mjini Songea,Kanali Abbas amesema akiwa katika ziara ya kikazi wilayani Tunduru hivi karibuni aliweza kutembelea masoko ya madini ya  vito ambayo ni soko la Generation,TUDECU na kukagua ujenzi wa soko jipya la madini.

Amesema akiwa katika masoko ya madini ya Generation na TUDECU walijitokeza wananchi wengi ambao walitaka kupata ufafanuzi wa baadhi ya kero zinazowasumbua ambapo baadhi ya wananchi walijitambulisha kuwa ni wafanya biashara wa madini ya vito wilayani Tunduru.

Amesema wafanyabiashara hao waliiomba serikali kuwatafutia fursa za mikopo kwenye Taasisi za fedha ili waweze kufanya biashara za madini kwa ufanisi mkubwa.

Ameongeza kuwa wafanyabiashara hao pia walikuwa na hoja ya kutaka majibu ya serikali ni juu ya uwepo wa  masoko Zaidi ya moja ya uuzaji wa madini ya vito wilayani humo.

“Kwa ugeni wangu niliona masuala haya hayahitaji majibu ya haraka,niliwashauri wanipe muda ili niweze kuwapatia majibu,leo nimewaita wanahabari kuwajulisha kwamba,jambo hilo serikali inalifanyia kazi kwa kuwa ni jambo linalohitaji utafiti mkubwa na majibu mazuri’’,alisisitiza Kanali Abbas.

Kutokana na hali hiyo Mkuu wa Mkoa amesema aliamua kuunda Tume maalum ya wataalam ambayo itakwenda kufanya utafiti wa hoja zote hizo ili majibu  yatakayorudi yaweze kutoa maamuzi  ya serikali juu ya uwepo wa soko moja au  masoko matatu  ya madini wilayani Tunduru.

Amesisitiza kuwa msimamo wa serikali utatolewa baada ya timu hiyo maalum kukamilisha kazi yake na kuleta majibu  ndani ya siku saba.

Wilaya ya Tunduru ina utajiri wa karibu aina zote za madini ya vito isipokuwa madini ya tanzanite ambayo katika dunia nzima yanapatikana Mirerani mkoani Manyara.

Madini mengine yenye thamani kubwa aina ya shaba yamegundulika katika Kata ya Mbesa Tarafa ya Nalasi wilayani Tunduru.

Kugundulika kwa madini hayo kunaifanya wilaya ya Tunduru kuwa ndiyo wilaya pekee nchini na Afrika Mashariki na Kati kuwa na madini ya shaba mbalimbali zikiwemo kijani,bluu na njano.

Utafiti unaonesha kuwa Tarafa nzima ya Nalasi ina utajiri wa madini hayo ambayo yanaweza kuchangia kuinua uchumi wa wilaya hiyo,Mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla wake.

Utafiti wa awali umebaini madini hayo yameenea hadi mto Ruvuma mpakani na nchi jirani ya Msumbiji na pia madini hayo yamesambaa hadi mpakani na wilaya ya Namtumbo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.