• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI ilivyodhamiria kuzinufaisha kaya masikini

Imewekwa kuanzia tarehe: July 11th, 2023

Akiongea kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Mchomoro wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma Mwezeshaji  Edigna Muhule ambaye pia ni afisa mifugo wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo alitoa kauli ya marufuku kwa wanufaika wa kaya maskini kutumia vibarua katika ajira ya muda inayotolewa na Tasaf .

Muhule aliwafafanulia wananchi lengo la serikali la kuweka ajira ya muda kwa wanufaika wa fedha za kaya maskini ni kuwaongezea kipato hivyo kitendo cha wanufaika hao kuwaajiri vibarua kuwafanyia kazi ni kinyume na malengo ya serikali.

Hata hivyo Muhule alidai serikali kupitia utekelezaji wa miradi mipya inakuja na utaratibu wa kuwatambua wanufaika wa kaya maskini ambao hawawezi kufanya kazi za ajira za muda kulingana na umri wao hao wataendelea kupokea fedha ya kumtambua kuwa kaya maskini pamoja wategemezi wake kama awali lakini wanufaika wale wenye uwezo wa kufanya kazi watafanya kazi za muda hawatahusika na kile kiasi walichokuwa wanapokea awali kwa kuwa ajira ya muda itawapatia fedha za kutosha kupitia kazi wanazofanya huku wategemezi wakibaki na malipo yao kama wanasoma shule .

Mratibu wa Tasaf wilaya ya Namtumbo Hyasint Mbiro alisema utambulishaji wa miradi mipya ya Tasaf wilayani Namtumbo ina enda sambamba na utoaji elimu ya namna miradi hiyo itakavyotekelezwa kwa kupitia wanufaika wa fedha za kaya maskini Tasaf ili waweze kujiongezea kipato.

Mbiro aliwataka wanufaika wa kaya maskini kujitokeza kufanya kazi ya ajira ya muda ili kujiongezea kipato kwa kuwa ajira hiyo ndiyo inawawezesha kupata fedha nyingi ukilinganisha na ruzuku wanazolipwa.

Pamoja na hayo Mbiro aliwataka wanufaika wa kaya maskini kuhakikisha anahudhuria kazini siku zote za kazi na kuwahimiza kuandika mahudhurio mara baada ya muda wa kazi kumalizika na kutojiorodhesha katika daftari la mahudhurio ukiwa kazini kutawakosesha fedha alisema Mbiro.

Saidi Ntali mnufaika wa fedha za kaya maskini  kijiji cha Mchomoro alionesha wasiwasi wake kwa mwezeshaji huyo kuwa bila kufanya kazi fedha za kila mwezi walizokuwa wakipata zitaenda wapi alisema Ntali.

Adamu Zuberi mnufaika wa kaya maskini kijiji cha Mchomoro aliwashukuru wawezeshaji na wataalamu kutoka ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri wilaya ya Namtumbo kwa kuwafafanulia utaratibu na mwongozo wa malipo ya Tasaf na kuondoa sintofahamu ambayo ilianza kujitokeza katika malipo ya Tasaf kutokana na kukosa uelewa wa namna malipo hayo nyanavyofanyika badala ya kuwalaamu viongozi wao.

Zuberi aliwaomba wataalamu kutochoka kutoa elimu hiyo kwa wanufaika hao kwa kuwa wakati mwingine watu hulalamika kutokana na kukosa uelewa utaratibu na kuhisi kuibiwa .

Katika kijiji cha mchomoro Tasaf imetambulisha mradi mpya wa kujenga kivuko badala ya mradi wa visima sita katika kijiji hicho kuelekea katika hatua za mwisho za ukamilishaji.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.