• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yaagiza mazao yanayouzwa kwa stakabadhi za ghala yaongezwe

Imewekwa kuanzia tarehe: September 26th, 2022

SERIKALI imeiagiza Bodi ya  Usimamizi wa Mfumo wa  Sitakabadhi za Ghala kuhakikisha inaongeza idadi ya mazao yanayonunuliwa kupitia mfumo huo kutokana na kuwepo manufaa makubwa kwa mkulima na Taifa kwa ujumla.

Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Uwekezaji,Viwanda na Biashara Mhe.Exaud Kigaghe(MB) wakati anazindua  na kufunga mafunzo ya siku tatu kwa Waendesha Ghala kutoka mikoa mbalimbali nchini  yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Chuo Kikuu cha SAUT Tawi la Mtwara.

Amesema licha ya kuwepo changamoto chache katika utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi za Ghala hapa nchini,serikali inatambua manufaa makubwa ya mfumo huo ambayo ameyataja kuwa ni mkulima kupata ulinzi sokoni na kunufaika na uzalishaji wake kwa kupata bei stahiki sokoni.

“Mfumo huu umekuwa kichocheo cha ukuzaji wa ajira rasmi na ajira zisizo rasmi hususan katika maeneo ya vijijini,mfumo umeleta tija ndiyo maana serikali imetoa agizo kwa Bodi  kuhakikisha kuwa inaeneza mfumo huu kwenye mazao karibu yote katika nchi hii yakiwemo mazao ya chai,pamba,tumbaku na bidhaa nyingine ambazo sio za kilimo ili mradi ziwe na tija kupitia mfumo huu’’,alisisitiza Mhe.Kigaghe.

Ameyataja mafanikio mengine ya mfumo huo kuwa ni ongezeko la bei  za mazao ambapo mapato ya Mkulima na serikali yameongezeka kwa wastani wa asilimia 200,ongezeko la uzalishaji wa mazao umeongezeka kwa wastani wa asilimia 12 kwa mwaka na upatikanaji wa takwimu sahihi za mazao yanayopita kwenye mfumo wa stakabadhi za ghala.

Amesema mfumo huo pia umeongeza mapato ya uhakika kwa serikali Kuu na Serikali za Mitaa sanjari na kukuza huduma za fedha vijijini na kwamba mfumo unachochea ajira ambapo katika Kwa mujibu wa Naibu Waziri,msimu wa mwaka 2021/2022 kwenye zao la korosho pekee ghala 34 zilisajiriwa  na kuwezesha kutoa ajira 1,258.

Hata hivyo amesema kati ya ajira hizo  mfumo umetoa ajira rasmi 284 za wasimamizi wa Ghala na ajira zisizo rasmi 680 za wachukuzi mzigo,watoa huduma za chakula 340 na tripu za malori 23,000 za kupeleka na kutoa mzigo ghalani.

Akitoa taarifa mafunzo hayo,Kaimu Mkurugenzi Bodi ya Usimamizi Stakabadhi za Ghala nchini Asangye Bangu amelitaja lengo ya mafunzo hayo kuwa ni kutoa elimu na kujenga uelewa wa Pamoja katika kutumia njia za kisasa na zenye tija katika usimamizi wa ghala unaowezesha uuzaji  zao la korosho kabla ya msimu kuanza Oktoba mwaka huu.

Hata hivyo amesema ghala zinajumuisha za watu binafsi serikali,Taasisi za Umma,ghala kuu za vyama vikuu vya ushirika na ghala za vyama vya msingi na mafunzo yatatua changamoto zilizopo kwenye mfumo ikiwemo masuala ya ubora wa mazao,upotevu wa mazao yakiwa ghalani na matumizi sahihi ya mizani.

Amezitaja mada ambazo zimefundishwa kwenye mafunzo hayo kuwa ni elimu ya mfumo wa stakabadhi Ghala,tathimini ya msimu wa korosho 2021/2022,matumizi ya vipimo vya unyevu ghalani na matumizi sahihi ya mizani ghalani.

Mada nyingine amezitaja kuwa  ni matumizi ya mfumo wa usimamizi wa ghala kwa TEHAMA,miongozo ya usimamizi wa mazao ghalani,taratibu za kutunza kumbukumbu ghalani,sheria na kanuni zinazosimamia mfumo.

Mafunzo kwa waendesha Ghala yamekuwa yanatolewa kila mwaka kabla ya msimu wa zao la korosho kuanza ili Waendesha Ghala watambua sheria zinazosimamia utekelezaji wa mazao  ya ghala.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari  Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Septemba 25,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.