• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yapongezwa kwa ujenzi wa maghala ya kuhifadhia nafaka

Imewekwa kuanzia tarehe: September 12th, 2021

WADAU wa kilimo katika Halmashauri ya wilaya ya Songea mkoani Ruvuma,wameipongeza serikali kwa hatua iliyochukua ya kuanza kuelekeza fedha kwa ajili ya ukamilishwaji wa miradi ya kilimo ikiwemo ya ujenzi wa ghala la kuhifadhia nafaka katika kata ya Magagura wilayani humo ambayo ilifanyiwa ufuatiliaji na asasi ya millenium Arts group na kuonekana kuwa na changamoto ya kushindwa kukamilika kwa muda mrefu na kutoa tija kwa wananchi. 

Pongezi hizo zilitolewa hivi karibuni na Afisa pembejeo wa Halmashauri hiyo  Ephraim Nyakunga wakati alipokuwa akichangia hoja katika mafunzo ya utawala Bora na ufuatiliaji wa rasilimali za umma(PETS)yaliyoandaliwa na asasi hiyo kupitia ufadhili wa The Foundation For Civil Society.

Nyakunga alisema kuwa tangu asasi hiyo ianze kutekeleza mradi wa utawala Bora na ufuatiliaji wa rasilimali za umma katika kata nane za Halmashauri hiyo matokeo chanya yameanza kuonekana ikiwa pamoja na serikali kuchukua hatua ya kuelekeza fedha kwa ajili ya ukamilishwaji wa mradi wa ujenzi wa ghala la kuhifadhia nafaka katika kata ya Magagura wilayani humo.

Aidha alisema kuwa Halmashauri hiyo pia imeweza kufanya maboresho kwenye baadhi ya maeneo ambayo yalionekana kuwa na changamoto wakati wa ugawaji wa pembejeo za Ruzuku za kwa msimu uliopita baada ya asasi hiyo kufanya ufuatiliaji kwenye miradi ya sekta ya kilimo wilayani humo.

Awali kaimu mkurugenzi wa Halmashauri hiyo John Mosha akifungua mafunzo hayo ameipongeza asasi hiyo ya Millenium Arts Group kwa kuchochea kasi ya maendeleo ambapo ameiagiza Idara ya mipango na kilimo kuendelea kutoa ushirikiano kwa asasi hiyo.

Akizungumza katika mafunzo hayo mkurugenzi mtendaji wa asasi hiyo Mnung’a Shaib Mnung’a alisema kuwa mradi huo wa utawala Bora unatekelezwa katika kata nane za Magagura,Kizuka,Mpitimbi,Litapwasi,Peramiho,Litisha,Muhukuru na Lilahi kwa kipindi cha miezi nane kwa gharama ya shilingi milioni 42 za kitanzania lengo likiwa ni kupata matokeo chanya katika miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake mshauri mwelekezi katika masuala ya utawala Bora Lawrence Chuma alisema kuwa changamoto kubwa inayojitokeza kwa Nchi nzima ni kukosekana kwa uwajibikaji,uwazi na ushirikishwaji kati ya viongozi na wananchi  katika shughuli za maendeleo.

Imeandikwa na Julius Konala


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.