• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa bilioni 1.4 kujenga shule mpya tatu Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: December 5th, 2022

SERIKALI ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetoa shilingi bilioni 1.4 kujenga shule mpya tatu za sekondari katika wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa shule hizo uliofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas,Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Dkt.Julius Lingu amezitaja shule hizo kuwa ni Nakayaya,Majimaji na Lumbukule.

Amesema shule hizo zinajengwa kupitia Programu ya Uboreshaji Elimu ya Sekondari nchini (SEQUIP) ambapo kila shule imepewa shilingi milioni 470 kutekeleza mradi huo.

“Ujenzi wa shule hizo bado unaendelea,kuna mapungufu ambayo yamejitokeza katika ukaguzi uliofanywa na Mkuu wa Mkoa hivyo mapungufu hayo yatafanyiwa kazi  na kufanyiwa marekebisho ili shule hizo ziweze kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza ifikapo Januari 2023’’,alisisitiza.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tunduru Chiza Marando  ameyataja majengo yanayojengwa katika kila shule kuwa ni ujenzi wa maabara tatu,vyumba nane vya madarasa,matundu 20 ya vyoo,jengo la utawala,minara miwili ya maji,jengo la TEHAMA na jengo la maktaba.

Akizungumza mara baada ya kukagua shule hizo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa shilingi bilioni 7.7 kutekeleza ujenzi wa shule mpya 11 za sekondari mkoani Ruvuma.

Kati ya shule hizo mpya, shule tatu zinajengwa katika wilaya ya Tunduru hivyo RC Thomas amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kusimamia ujenzi wa shule hizo na kuweka samani zake katika kila darasa  ili shule hizo zianze kuchukua wanafunzi  Januari 2023.

“Mhe.Rais alishamaliza kazi yake ya kututafutia pesa  kutuletea hivyo ni wajibu wetu sisi sote kama timu kusimamia na kuhakikisha miradi  ya serikali inatekelezwa kwa viwango na thamani inayolingana na fedha’’,alisisitiza.

Serikali Kuu kupitia  Programu ya Uboreshaji wa Elimu ya Sekondari nchini (SEQUIP) inajenga shule mpya za sekondari 1000 katika nchi nzima,kati ya hizo shule 11 zinajengwa katika Mkoa wa Ruvuma.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Novemba 5,2023

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.