• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa bilioni 16 kutekeleza miradi ya maji Mkoa wa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: July 29th, 2020

SERIKALI ya awamu ya tano imetoa zaidi ya shilingi bilioni 16 kutekeleza miradi mbalimbali ya maji mkoani Ruvuma hali iliyoweza wananchi 1,149,867  kupata maji safi na salama hadi kufikia mwaka huu.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema idadi ya wananchi wanaopata  huduma ya maji safi na salama katika Mkoa wa Ruvuma hivi sasa ni asilimia 63.9 ya wakazi wote wa Mkoa idadi ambayo imeongezeka kutoka asilimia 57 ya wananchi waliokuwa wakipata huduma hiyo mwaka 2015. 

Hata hivyo Mndeme amewataja wananchi wanaoishi maeneo ya vijijini wanaopata huduma ya maji safi na salama wanakadiriwa kuwa 888,005 ambao ni sawa na asilimia 61.6,ambao wanapata  maji kupitia vituo vya kuchotea maji 5,631.

“Katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama na kufikia malengo ya kitaifa, Mhe, Rais ameendelea kuwezesha  ukarabati na ujenzi wa miradi mipya ya maji, kuanzisha na kusajili kisheria jumuiya za watumia maji vijijini kwa ajili ya kusimamia na kuendesha miradi ya maji’’,alisema.

 

Kuhusu huduma ya maji mijini,Mkuu wa Mkoa amesema Mkoa wa Ruvuma una miji sita ambayo ni makao makuu ya Halmashauri ukiwepo mji wa Songea ambao ni makao makuu ya Mkoa. Miji hiyo ni Songea, Mbinga, Tunduru, Namtumbo, Mbambabay na Madaba.

Mndeme amesema Hadi kufikia mwaka 2020 hupatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika Manispaa ya Songea umefikia asilimia 91 ikilinganishwa na asilimia 72.7 kwa mwaka 2015.

Ameutaja Mpango wa utekelezaji miradi ya maji vijijini katika mwaka wa fedha 2019/2020,serikali imeupatia Mkoa wa Ruvuma kiasi cha shilingi 1,168,888,500.83 kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa miradi 29 ya maji.

Mndeme amesema katika kipindi cha mwaka 2019/2020,serikali imeupatia Mkoa wa Ruvuma shilingi  bilioni 7.8 kwa ajili ya Kujenga, kukarabati na kufanya upanuzi katika miradi 33 ya maji katika wilaya zote tano .

Akizungumzia hali ya utekelezaji wa miradi kupitia programu ya lipa kwa matokeo na Mfuko wa Maji,Mkuu wa Mkoa amesema hadi kufikia mwaka 2020 Kupitia Program ya lipa kwa matokeo , Jumla ya miradi 19 imekamilika,miradi kumi inaendelea kutekelezwa na miradi 33 iko kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji.

Ameongeza kuwa katika kukabiliana na tatizo la maji, Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kujenga na kukarabati miundombinu ya maji na kupanua mitandao ya maji ili kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama.

 Maelekezo ya Ilani ya CCM ya mwaka 2015 ni kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama vijijini unaongezeka toka asilimia 67.7 mwaka 2015 na kufikia asilimia 85 mwaka 2020; miji ya makao makuu ya Mikoa toka asilimia 68 mwaka 2015 na kufikia asilimia 95 mwaka 2020 na miji mikuu ya Wilaya na miji midogo toka asilimia 57 mwaka 2015 hadi asilimia 90 mwaka 2020.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 29,2020

 

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.