• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa milioni 200 kuanza ujenzi wa kituo cha afya Kingerikiti Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: March 1st, 2020

Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa,  inatarajia kuanza ujenzi wa Kituo cha afya katika Kata ya  Kingerikiti, tarafa ya Mpepo, Kwa Lengo la kutatua kero ya wananchi wa kata hiyo waliokuwa wakisafiri umbari mrefu wa takriban Kilometa arobaini (40), kufuata huduma za matibabu katika Wilaya ya Mbinga.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Nyasa Bw. Jimson Mhagama,  jana wakati akiongea na wananchi wa Kata ya Kingerikiti kwa lengo la kutambulisha mradi na kuwashirikisha Wananchi  ili waweze kushirikiana na Serikali kwa lengo la kutekeleza Mradi huo.

Mhagama alifafanua kuwa, Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa imepokea Shilingi milioni mia mbili tu (Tsh 200,000,000/=) toka Serikali kuu kwa lengo la kujenga kituo cha afya cha Kingerikiti, ili kuwaletea huduma karibu za matibabu kwa wananchi wa kata hiyo, hivyo kwanza kabisa wananchi mnatakiwa kufahamu mradi huu na kushirikiana na Serikali  kuhakikisha ujenzi huu unakamilika ndani ya miezi miwili kuanzia sasa.

Mhagama aliongeza kuwa Serikali imedhamiria kuboresha miundombinu ya Afya katika Wilaya ya Nyasa kwa kuhakikisha inatatua matatizo ya wananchi, hususani kwenye sekta ya afya, kwa kushirikiana na wananchi wa sehemu husika kwa kuangalia jiografia ya Wilaya.

Kwa upande wao Wananchi wa Kata ya Kingerikiti walimpongeza Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli, na Mh. Mbunge wa Jimbo la Nyasa, Mhandisi Stella Manyanya ambaye ni Naibu waziri wa Viwanda na Biashara kwa kutekeleza ahadi yake kwa kuwa aliahidi na ametekeleza ahadi yake ya kuwajengea Kituo cha afya  cha Kingerikiti.

“Sisi wananchi wa Kata ya Kingerikiti,  tumeupokea mradi huu na tunampongeza sana Mbunge wetu na Mh, Rais John Magufuli kwa kutujengea Kituo cha afya katika kata yetu kwa kuwa tulikuwa tunatembea umbali mrefu wa takribani kilometa 40  kufuata huduma za afya katika Hospitali ya Litembo iliyoko wilayani Mbinga au Hospitali ya Wilaya ya Mbinga, hivyo tupewe majukumu yetu na tutahamasishana ili Ujenzi huu utekelezwe kwa muda uliopangwa.” alisema Wiligs ndunguru mkazi wa kijiji cha Kingerikiti kwa niaba ya wananchi wote.

Mganga mkuu wa Wilaya ya Nyasa Dkt Aaron Hyera, aliwaambia wananchi kuwa mara baada ya kukamilika kwa kituo hicho cha afya cha kingerikiti kwa jiografia ya Wilaya ya Nyasa, huduma za afya zitatolewa vizuri kwa kuwa wagonjwa watakuwa hawatembei umbali mrefu na kupata huduma kwa wakati. Aliwataka wananchi hao kushiriki kikamilifu kujenga kituo hicho cha afya ambacho kipo katika Tarafa ya Mpepo na kwa sasa Tarafa ya Mpepo itakuwa na Vituo viwili vya Afya vya Serikali ambavyo ni Liparamba na Kingerikiti.

Aidha uboreshajiwa sekta ya afya katika Wilaya ya Nyasa umeimarika kwa kukamilika kwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya, iliyojengwa Kijiji cha Nangombo Kata ya Kilosa Tarafa ya Ruhekei na Vituo vya  Afya Kihagara,Mbambabay na Mkili vitafanya idadi ya Vituo Vya Afya kuwa Vitano (05) kitakapokamilika kituo cha Afya cha Kingerikiti.

Imeandaliwa

Na Netho C. Sichali

Kaimu Afisa habari  (W) Nyasa

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.