• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa milioni 560 kujenga sekondari mpya Kata ya Upolo Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: October 20th, 2023

Mafundi  wameiomba kamati ya ujenzi wa shule mpya ya sekondari  kata ya Upolo Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma kuwaongezea muda wa utekelezaji wa mradi huo kutokana na miundombinu mibovu ya barabara wakati wa kusomba vifaa vya ujenzi.

Akizungumza wakati akisoma taarifa mbele ya kamati ya siasa CCM Mkoa wa Ruvuma Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Khalid Kharif amesema mafundi wameomba kuongezewa muda kutokana na changamoto mbalimbali zilizojitokeza ikiwemo ya  ukatikaji wa madaraja ya miti kwenye mito wakati wa kusomba vifaa vya ujenzi.

Amesema ujenzi huo unahusisha majengo ya vyumba vya madarasa nane, jengo la maabara, utawala, maktaba na Tehama, ambapo hadi mradi kukamilika utagharimu kiasi cha fedha zaidi ya shilingi milioni  560 iliyotoka  Serikali kuu kupitia mradi wa SEQUIP.

Kharif amesema mradi ulianza kutekelezwa Agosti 14 2023 na ulitarajiwa kukamilishwa Septemba 2023 ambapo sasa mradi unatarajia kukamilika Oktoba 30 mwaka huu.

 “Wananchi wameshiriki kufanya kazi za kukusanya mawe tripu 18 na kujaza kifusi ndani kwenye msingi tripu 64 kwa kazi hizo zinathamani ya kiasi cha fedha shilingi 3,880,000.00”, amesema Kharif.

Amezitaja changamoto wanazokumbana nazo kuwa ni Maji yaliyopo hayatoshelezi miundombinu mibovu ya madaraja ya mito ambayo yanatuunganisha na Wilaya ya Mbinga ambapo tunachukulia  vifaa vya ujenzi na

Hata hivyo amesema kati ya fedha shilingi milioni 560 mpaka sasa zimetumika zaidi ya shilingi milioni 123 na wamebakiwa na kiasi cha fedha zaidi ya  shilingi milioni  437.

Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma ikiongozwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma Ndugu Mohamed Ally imeridhishwa na utekelezaji wa mradi huo wa sekondari mpya ambapo wameagiza channgamoto zilizopo zipatiwe ufumbuzi wa haraka ili mradi uweze kukamilika.

Imeandikwa na Farida Baruti 

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 20,2023

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.