• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

Imewekwa kuanzia tarehe: June 1st, 2025

 TANZANIA inahitaji uwekezaji zaidi wa mashamba makubwa ili kufungua fursa ya ajira kupitia kilimo kama ilivyokuwa kwa shamba kubwa la kahawa Afrika Mashariki la Aviv Tanzania Limited lililopo katika Kijiji cha Lipokela Wilayani Songea Mkoani Ruvuma.

Shamba la AVIV lina ukubwa wa hekta zaidi ya 2000 na linazalisha kahawa yenye ubora  wa hali ya juu hali inayosababisha Tanzania kusomeka vema kwenye ramani ya dunia kwa kuwa na Kahawa bora.

Shamba hilo ni Muhimu kwa Taifa kwa kuwa limetoa ajira kwa Wananchi wa Mikoa mbalimbali nchini ikiwemo ya Ruvuma na Mtwara na kusaidia fedha za kigeni Nchini kwa kuwa wanauza kahawa yao moja kwa moja nje ya Nchi.


Meneja Msaidizi wa Kampuni ya Aviv Tanzania Muthana Maruvanda amesema Kampuni hiyo kupitia Shamba lao la Kahawa imedhamiria kukuza zao la kahawa kwa miundombinu bora ya umwagiliaji ambayo Wakulima wa kahawa Mkoani Ruvuma wanajifunza kilimo cha kisasa kupitia Shamba hilo.

Naye Meneja wa Shamba la Kahawa la Aviv,Hamza Kassim amesema shamba hilo linachangia Asilimia 4.5 ya Kahawa yote inayozalishwa Nchini .

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan Septemba 2024 alitembelea shamba la AVIV ambapo alisema mafanikio yaliyopo sekta ya kilimo hayatokei kwa bahati mbaya bali ni kutokana na juhudi kubwa zilizofanywa na serikali.


Alisema zao la kahawa pekee limeongezeka katika uzalishaji kutoka tani 65 hadi kufikia tani 85,hivyo kuingiza dola milioni 250 nchini.

Katika hatua nyingine, Rais Samia ameutaka uongozi wa shamba hilo,kufanya shughuli za kijamii,ujikite katika uchimbaji wa visima vya umwagiliaji kwenye mashamba ya wakulima.


Mafanikio yaliyopo  katika sekta ya kilimo yametokana na maamuzi ya kisera na sheria ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hususani katika kuboresha sekta ya uwekezaji na kurudisha masoko.


 Shamba la AVIV Tanzania Ltd ni moja kati ya mashamba 50 makubwa yanayozalisha kahawa nchini, likiwa na zaidi ya hekta 2,000, ambapo zaidi ya hekta 1,000 zimeshapandwa kahawa na kwamba asilimia 60 ya kahawa inayozalishwa na shamba hilo inauzwa nje ya nchi.

Uzalishaji wa kahawa umeongezeka kutoka tani 60 hadi kufikia tani 85 na kwamba shamba hilo pia limeanza kuotesha pilipili manga (black pepper) na kuuza nje ya nchi, likiwa na uzalishaji wa tani mbili na lengo la kufikia tani tatu.

Shamba la kahawa la Kampuni ya AVIV lina ukubwa wa hekta 2,000, ambapo hekta 1,000 zimetumika kwa uzalishaji wa kahawa. Linatoa ajira za kudumu 1,400 na ajira za msimu 5,000.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DKT Nchimbi awaongozawananchi kuuaga mwili wa Mzee Songambele

    June 02, 2025
  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.