TANZANIA inahitaji uwekezaji zaidi wa mashamba makubwa ili kufungua fursa ya ajira kupitia kilimo kama ilivyokuwa kwa shamba kubwa la kahawa Afrika Mashariki la Aviv Tanzania Limited lililopo katika Kijiji cha Lipokela Wilayani Songea Mkoani Ruvuma.
Shamba la AVIV lina ukubwa wa hekta zaidi ya 2000 na linazalisha kahawa yenye ubora wa hali ya juu hali inayosababisha Tanzania kusomeka vema kwenye ramani ya dunia kwa kuwa na Kahawa bora.
Shamba hilo ni Muhimu kwa Taifa kwa kuwa limetoa ajira kwa Wananchi wa Mikoa mbalimbali nchini ikiwemo ya Ruvuma na Mtwara na kusaidia fedha za kigeni Nchini kwa kuwa wanauza kahawa yao moja kwa moja nje ya Nchi.
Meneja Msaidizi wa Kampuni ya Aviv Tanzania Muthana Maruvanda amesema Kampuni hiyo kupitia Shamba lao la Kahawa imedhamiria kukuza zao la kahawa kwa miundombinu bora ya umwagiliaji ambayo Wakulima wa kahawa Mkoani Ruvuma wanajifunza kilimo cha kisasa kupitia Shamba hilo.
Naye Meneja wa Shamba la Kahawa la Aviv,Hamza Kassim amesema shamba hilo linachangia Asilimia 4.5 ya Kahawa yote inayozalishwa Nchini .
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan Septemba 2024 alitembelea shamba la AVIV ambapo alisema mafanikio yaliyopo sekta ya kilimo hayatokei kwa bahati mbaya bali ni kutokana na juhudi kubwa zilizofanywa na serikali.
Alisema zao la kahawa pekee limeongezeka katika uzalishaji kutoka tani 65 hadi kufikia tani 85,hivyo kuingiza dola milioni 250 nchini.
Katika hatua nyingine, Rais Samia ameutaka uongozi wa shamba hilo,kufanya shughuli za kijamii,ujikite katika uchimbaji wa visima vya umwagiliaji kwenye mashamba ya wakulima.
Mafanikio yaliyopo katika sekta ya kilimo yametokana na maamuzi ya kisera na sheria ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hususani katika kuboresha sekta ya uwekezaji na kurudisha masoko.
Shamba la AVIV Tanzania Ltd ni moja kati ya mashamba 50 makubwa yanayozalisha kahawa nchini, likiwa na zaidi ya hekta 2,000, ambapo zaidi ya hekta 1,000 zimeshapandwa kahawa na kwamba asilimia 60 ya kahawa inayozalishwa na shamba hilo inauzwa nje ya nchi.
Uzalishaji wa kahawa umeongezeka kutoka tani 60 hadi kufikia tani 85 na kwamba shamba hilo pia limeanza kuotesha pilipili manga (black pepper) na kuuza nje ya nchi, likiwa na uzalishaji wa tani mbili na lengo la kufikia tani tatu.
Shamba la kahawa la Kampuni ya AVIV lina ukubwa wa hekta 2,000, ambapo hekta 1,000 zimetumika kwa uzalishaji wa kahawa. Linatoa ajira za kudumu 1,400 na ajira za msimu 5,000.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.