• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SHIRIKA LA Compasion International latoa msaada wa vyandarua 250 kwa watoto wenye mazingira magumu Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: July 8th, 2020

 SHIRIKA la Compasion International lenye makao makuu yake jijini Arusha limetoa msaada wa vyandarua 250 vyenye thamani ya shilingi milioni  2.5  kwa Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Agustino Mji mwema Dayosisi ya Ruvuma.

 Msaada huo umetolewa kwa watoto wanoaishi katika mazingira magumu ili kujikinga na ugonjwa wa Malaria.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Anglikana Mjimwema Padre John Midelo amesema kati ya vyandarua hivyo,kituo cha Mjimwema kipata vyandarua 150 na kituo cha Lupapila kimepata vyandarua 100.

Mgeni rasmi katika hafla ya ugawaji wa vyandarua hivyo alikuwa ni  Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Songea  Afrosina Mwanja ambaye amewaasa wazazi na walezi kuwalea watoto katika maadili mazuri kwa sababu watoto hao ni viongozi wa baada.

Mwanja pia amewataka wazazi na walezi kuhakikisha kuwa  vyandarua vilivyotolewa vinatumika kwa watoto na siyo kwa wageni au watu wengine.

,,Akina mama na akina Baba tuwajali watoto tuondokane na mila kwamba tukiweka chakula mezani wale wakubwa mtoto atakula baadae, kunawa mkubwa mtoto anakuwa wa mwisho anakula uchafu hizo ni mila mbaya kwa watoto’’,alisisitiza.

Hata hivyo Mwanja ametoa  rai kwa wazazi kuhakikisha  watoto  wao wanapata haki  zao zote msingi ili waweze kuwa na maisha bora na kujenga taifa lenye maadili .

 Meneja wa CRDB B amechangia kituo hicho kiasi cha  200,000 kila mwezi kuanzia mwezi Juni hadi Desemba 2020 ambako ameagiza  fedha hiyo itumike kwa watoto hao wanaolelewa katika kituo hicho ili kutatua changamoto zao mbalimbali.

Kwa upande wake Meneja wa Benki ya NMB tawi la Songea ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kugawa vyandarua 100 katika kituo cha Lupapila amewaasa wazazi na walezi kuwajali na kuwasomesha watoto wao ili wapate elimu ambayo ndiyo urithi wa pekee katika maisha yao.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo Mchungaji Kiongozi  wa Kanisa hilo Padre John Midelo amelishukuru   shirika la Compasion International linaloshirikiana na Makanisa ya kipentecoste na CCT kulea  watoto katika Nyanja kuu nne Kiroho,Kimwili,Kiakili na kiuchumi.

Amesema watoto hao wanalelewa kuanzia umri wa miaka mitatu hadi sabaambao wanalelewa mpaka kufikia umri wa miaka 22  na kwamba  mtoto atakayeendelea na masomo ya juu ataendelea kufadhiliwa  mpaka chuo kikuu akiwa hajavuka miaka 22.

Padre Midelo amesema shirika hilo limeahidi kutoa bima ya afya watoto hao wanaoishi katika mazingira magumu watapewa bima ya afya na mavazi,vifaa vya shule na chakula.

Hata hivyo amesema  kituo hicho kinakabiliwa na changamoto ya miundo mbinu ambapo hadi sasa watoto wanaosoma idadi yao ni 95 na kwamba wana upungufu wa madarasa  na choo kimejengwa kwa gharama milioni saba lakini bado  ujenzi wake haujakamilika.

Mwenyekiti wa Kamati ya Wazazi Noela chisokole amelipongeza shirika hilo pamoja na makanisa yanayoshirikiana kutoa masaada huo kwa watoto wao,ambapo amesema awali hali ilikuwa ngumu kwa upande wa mavazi,chakula vifaa vya shule na matibabu.

 Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa habari kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa

Ruvuma songea

Julai 8,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.