Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Ruvuma imefanikiwa kuokoa zaidi shilingi milioni 9.2 ambazo ni sehemu ya mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2025.
Taarifa hiyo imetolewa na Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Janeth Haule wakati anazungumza na wanahabari ofisini kwake Mahenge mjini Songea
Amesema fedha hizo zilikusanywa na mawakala kupitia mifumo ya kielektroniki na ziliwasilishwa benki baada ya kufanyika kwa ufuatiliaji maalum.
Naibu Mkuu wa TAKUKURU amesema hatua hiyo pia imechochea ongezeko la makusanyo katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, biashara, pamoja na ardhi na maliasili kutoka asilimia 50 hadi 102.
Amesema Taasisi hiyo imetoa ushauri wa marekebisho katika miradi mitatu yenye thamani ya Zaidi ya shilingi milioni 29.9 katika sekta za miundombinu, kilimo na fedha kutokana na dosari zilizobainika.
Katika utekelezaji wa programu hiyo katika kata 12, jumla ya kero 118 zilibainika, ambapo 89 zimetatuliwa na 39 zinaendelea kufanyiwa kazi.
TAKUKURU imetoa RAI kwa wananchi kushiriki kikamilifu uchaguzi Mkuu wa 2025 kwa kuepuka vitendo vya rushwa.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.