• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TAKUKURU Ruvuma yaokoa zaidi ya milioni 554

Imewekwa kuanzia tarehe: April 18th, 2020

Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Ruvuma Imeokoa mifuko 100 ya saruji katika mradi wa ujenzi wa zahanati ya Masimeli katika Halmashauri ya Mji wa Mbinga.

Akitoa taarifa ya utendaji kazi wa  TAKUKURU katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Machi 2020,Mkuu wa TAKUKURU  Mkoa wa Ruvuma, Yustina Chagaka amesema Mifuko hiyo ilikuwa mbioni kuibiwa na baadhi ya viongozi wa kata ya kitanda katika Halmashauri hiyo.

Amesema baada ya TAKUKURU kubaini njama hizo iliamua mifuko hiyo ya saruji irejeshwe katika Halmashauri ya mji wa Mbinga.

 Chagaka amesema Halmashauri ya mji wa Mbinga ilipeleka saruji mifuko 120 kaitka mradi huo ambapo mahitaji ni mifuko 240 lakini kuna fedha ambayo ilitolewa na Mhisani kutoka Ujerumani kiasi cha Euro 10,000 sawa milioni 24  kwa kata ya Kitanda.

“Tumejipanga kuendelea kuelimisha wananchi kupiga vita rushwa katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwisho mwa mwaka 2020 ili wananchi wafahamu thamani ya kura zao na umuhimu wa kuchaguwa viongozi bora.” Amesema Chagaka.

Katika hatua nyingine, TAKUKURU wameokoa jumla ya fedha zaidi ya milioni 554,ambazo zimetokana na uchunguzi mbalimbali ambao unaendelea kufanywa na TAKUKURU.

Amesema kati ya fedha hizo zaidi ya milioni 498, zimeokolewa kutokana na uchunguzi  wa vyama vya kuweka na kukopa (SACCOS)Wilaya ya Songea.

Hata hivyo kiasi cha  fedha zaidi ya milioni 10,zimeokolewa kutokana na  uchunguzi uliofanyika katika vyama vya ushirika (AMCOS) Wilayani Namtumbo ambapo fedha hizo zimekabidhiwa kwa wakulima waliokuwa wamedhulumiwa mazao yao.

Chakaga amesema zaidi ya milioni 1.6 ,ni fedha ambazo zimerejeshwa baada ya uchunguzi katika mfuko wa TASAF Wilayani Tunduru baaada ya kubaini kwamba baadhi ya watumishi walikuwa wakijilipa posho isivyohalali.

Imeandikwa na Farida Mussa

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.