• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TAMASHA la Toyota Festival kutangaza vivutio vya Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: December 9th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma Peres Magiri amezindua Tamasha kubwa la Toyota Festival ambalo limelenga juhudi za kuimarisha utalii, kukuza uchumi wa Mkoa huo na kuhamasisha ushirikiano wa kijamii kupitia shughuli mbalimbali za kibiashara na kijamii.

Mkuu wa Wilaya huyo ambaye amemwakilisha mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed alisema hayo wakati wa uzinduzi wa Toyota Networking cocktail iliyofanyika Disemba 7mwaka huu kwenye ukumbi wa mikutano Anglikana manispaa ya Songea.

Alisema kuwa Tamasha hilo  ambalo linatarajia kuwa na maandamano ya magari aina ya Toyota zaidi ya 5000 kutoka Songea hadi Mbambabay wilayani Nyasa inatarajiwa kufanyika Juni 2025.

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Peres Magiri akizindua Tamasha la Toyota festival mkoani Ruvuma.

“Tamasha hilo litajumuisha maonesho ya magari ya Toyota ,shughuli za Burudani,maonesho ya bidhaa mbalimbali pamoja na fursa za kiuchumi kwa wananchi wa Mkoa wetu wa Ruvuma”alisema mkuu huyo wa Wilaya Magiri.

Alisema lengo la tamasha hilo ni kuhakikisha tamasha linakuwa na fursa nzuri ya kuonesha rasilimali za kiutalii na kiuchumi zinazo patikana katika Mkoa huo.

Hata hivyo amewakaribisha wawekezaji, Taasisi mbalimbali na wananchi kushiriki kwenye tamasha hilo ili kuongeza nafasi za ajira na kukuza maendeleo ya kiuchumi.

Kwa upande wake KatibuTawala wa Mkoa wa Ruvuma Mary Makondo amesema kuwa Tamasha la Toyota festival litasaidia kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo ndani ya Mkoa huo na kwamba  litakusanya watu kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania

. Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Mary Makondo akizungumza kwenye uzinduzi wa Tamasha la Toyota festival lililofanyika katika ukumbi wa mikutano Anglikana Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Alisema kuwa serikali inatumia magari aina ya Toyota hivyo wanawaharika  watu mbalimbali toka ndani na nje ya nchi kushiriki na kufadhili Tamasha hilo hivyo wawe mstari wa mbele kuhakikisha wanafanikisha.

“Ni imani yangu kuwa tutaendelea kushirikiana katika maandalizi ya Tamasha hili ili kutangaza utalii wa Mkoa wa Ruvuma ambalo linatarajiwa Kufanyika mwezi juni mwakani ambapo wadau mbalimbali wa utalii toka ndani na nje ya Mkoa wa Ruvuma wanakaribishwa kufadhili ,”Alisema Makondo.

Mwakilishi wa kampuni  ya Toyata Mkoa wa Ruvuma,Wakili John Njau alisema kuwa Toyota wameweza kuuza Magari na vipuri mbalimbali ambapo Tamasha hilo la Toyota festival ni Tamasha ambalo linawaweka wananchi pamoja na si vinginevyo.

Naye Kamanda wa wakala wa misitu (TFS )Kanda ya kusini Manisie  Mpokigwa,amesema kuwa Taasisi yake inafanya kazi ya kutangaza utalii wa vivutio mbalimbali hivyo Tamasha hilo litasaidia kutangaza utalii wa Mkoa wa Ruvuma ikiwemo Misitu ya hifadhi ya chanzo cha mto Ruvuma kilichop Milima ya Matogoro lakini pia wanautajiri wa hali ya juu katika mapori ya TANAPA na TAWA hivyo watalii wengi wameongezeka

Maajabu Mbogo muhifadhi toka TAWA, Mkoa wa Ruvuma amesema kuwa Mkoa wa Ruvuma umejaliwa vivutio vingi  vya utalii ikiwemo hifadhii ya Nyerere,kisiwa Cha Lundo ambapo Kuna samaki wa urembo zaidi ya 400, makumbusho ya maji maji ,fukwe za ziwa Nyasa,milima Matogoro,na vivutio vingine vingi.

Titos Kajungu ofisa Masoko toka kampuni ya Wategi wamekuja na wazo la kutangaza vivutio vya utalii vya Mkoa wa Ruvuma ambavyo ni vya kipekee na wameamua kuwa na mkakati mzuri  wa kushirikiana na Serikali kuendelea kuhamasisha utalii na  wataendelea kuvitangaza vivutio vilivyopo Mkoa wa Ruvuma ili wajue uzuri wa Mkoa na Nchi kwa ujumla.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.