• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANROADS Ruvuma yapongezwa kwa kukabiliana na maafa ya mvua kwenye mkiundombinu

Imewekwa kuanzia tarehe: March 3rd, 2020

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewapongeza Wakala wa Barabara TANROADS mkoani Ruvuma kwa kufanya kazi ya ziada ya kukabiliana na maafa katika miundombinu ya madaraja na barabara unaotokana na mvua nyingi zinazoendelea kunyesha katika mkoa mzima.

Mndeme ametoa pongezi hizo baada ya kukagua daraja la Lukumbo katika Kata ya Mtipwili wilayani Nyasa ambalo limekatika na kusababisha kero ya usaifiri na usafirishaji kwa wananchi wanaotumia barabara hiyo ambayo inakwenda hadi mpakani mwa nchi ya Msumbiji.

“TANROADS Ruvuma mnafanyakazi kubwa sana kwa sababu athari zinazoletwa na mvua katika Mkoa wetu ni kubwa sana,leo tupo Nyasa katika Daraja la Lukumbo,lakini hivi tunavyoongea TANROADS wapo Lukumbule Tunduru wanarudisha mawasiliano,TANROADS wapo Nalasi,wapo mawe ya bunduki,wapo Madaba,wapo daraja la Mnyamwaji wanarudisha mawasiliano,suala la athari za mvua hakuna wa kumnyoshea kidole’’,alisisitiza Mndeme.

Amesema TANROADS hivi sasa usiku na mchana wapo kazini ambapo amewapongeza kwa hatua ya haraka ya kurudisha mawasiliano katika daraja la Lukumbo ambapo ametoa rai kwa wananchi kuchukua tahadhari katika kipindi cha mvua nyingi hasa wanapopita katika madaraja,makalavati na kwenye mito.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Nyasa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhandisi Stella Manyanya licha ya kutoa pongezi kwa serikali kwa kuanza matengenezo ya daraja hilo ambalo lipo katika Jimbo lake,amesema barabara nyingi jimboni humo hivi sasa zimeharibika kutokana na mvua zinazoendelea .

Hata hivyo amesema TANROADS imejipanga vizuri katika matengenezo ya barabara hizo na kwamba fedha kwa ajili ya marekebisho na matengenezo zimetengwa.

Kutokana na umuhimu wa barabara hiyo ambayo ipo mpakani na nchi ya Msumbiji,Mhandisi Manyanya ametoa rai kwa serikali kupitia TANROADS  itengwe bajeti ya kutosha ili kujenga daraja bora kati ya mawili yaliyoharibika katika eneo hilo.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Machi 3,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • SEKONDARI ya Dkt.Samia alama ya maendeleo Namtumbo

    June 01, 2025
  • MUONEKANO wa baadhi ya majengo ya hospitali ya Manispaa ya Songea

    June 01, 2025
  • RUSHWA ni adui wa haki

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.