• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TARURA Namtumbo waanza kujenga barabara za mitaa kwa kiwango cha lami

Imewekwa kuanzia tarehe: August 13th, 2023

WAKALA wa barabara za mijini na vijijini (TARURA) wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma,imeanza kujenga barabara za lami za mitaa katika mji wa Namtumbo ikiwa ni mkakati wa Serikali ya awamu ya sita ya kuwavutia wawekezaji kwenda kuwekeza katika wilaya hiyo yenye utajiri mkubwa wa rasilimali ardhi na misitu.

Kwa mwaka wa fedha 2022/2023,serikali  kuu imeipatia Wakala wa barabara za mijini na vijijini(Tarura)Sh.milioni 890 kwa ajili ya kujenga barabara  yenye urefu wa kilomita 1.6 katika mji wa Namtumbo.

Aidha fedha hizo,zimetumika kufunga taa za barabarani zinazotumia umeme wa jua na kujenga mitaro ya kupitishia maji ya mvua kwenda katika maeneo husika ambayo awali yalilazimika kwenda kwenye makazi ya wananchi.

Hayo yamesemwa  na Meneja wa TARURA wilayani humo Mhandisi Fabian Lugalaba,wakati akitoa taarifa ya ujenzi wa barabara za mitaa  katika maeneo mbalimbali ya mji wa Namtumbo.

Alisema,lengo kuu  la kujenga  barabara hiyo ni kuwawezesha wananchi wa mji  wa Namtumbo kuwa  na mawasiliano ya uhakika kutoka kwenye maeneo  yao kwenda makao makuu ya wilaya zilipo ofisi ya Mkuu wa wilaya,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri na maeneo mengine ya huduma za kijamii.

Alisema,TARURA imeamua kujenga na kuimarisha miundombinu ya barabara katika mji huo ili kuiwezesha serikali kutoa huduma bora kwa wananchi na kuibua fursa za uwekezaji na kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja,wilaya ya Namtumbo na mkoa wa Ruvuma.

Kwa mujibu wake,kabla ya kujengwa kwa barabara hiyo mji wa Namtumbo ulikuwa na barabara ya lami yenye urefu wa kilomita 0.9 tangu wilaya hiyo ilipoanzishwa miaka 14 iliyopita,hivyo kuongezeka kwa barabara ya Namtumbo-shule imesaidia sana kurudisha hadhi ya mji huo.

Ameishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kuiongezea TARURA fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miundombinu ya barabara na kuhaidi kuwa,fedha zote zilizopelekwa zitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuchochea kukua kwa uchumi na maisha ya wananchi.

Lugalaba,amewataka wananchi kuhakikisha wanatunza barabara hizo zinazojengwa katika maeneo yao kwa kutozidisha uzito,kutomwaga mafuta,kufanya shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo kando kando ya barabara ili ziweze kudumu kwa muda mrefu.

Wakazi wa Namtumbo,wameipongeza serikali kupitia Tarura kujenga barabara hiyo ambayo imesaidia sana kuupundezesha mji huo na kuwawezesha kufanya shughuli zao za kujipatia kipato kwa masaa 24 tofauti na hapo awali.

Joseph Hokororo alisema,kabla ya barabara hiyo kujengwa kwa lami wakati wa masika kero kubwa ilikuwa matope mengi na hata majira ya kiangazi kulikuwa na vumbi kubwa lililoingia ndani ya nyumba na hivyo kuathiri sana afya zao.

Aliongeza kuwa,kujengwa kwa kiwango cha lami barabara hiyo kumesaidia maeneo yao kuwa na hadhi kubwa na hivyo kushawishi watu wengi kuhitaji maeneo kwa ajili ya makazi na shughuli nyingine za kiuchumi.

Hilal Mgawe alisema,uwepo wa mradi huo umesaidia sana vijana kupata ajira za muda na hivyo kupata fedha za kujikimu ambapo ameiomba serikali kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo itakwenda kuinua hali zao za maisha.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.