• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TARURA Ruvuma ilivyoboresha mtandao wa barabara na madaraja

Imewekwa kuanzia tarehe: March 22nd, 2023

MKOA wa Ruvuma una Jumla ya kilometa 4,130.63 za mtandao wa Barabara zinazosimamiwa na TARURA   ambazo hupitika kwa mwaka mzima.

Kwa Mujibu wa Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Wahabu Nyamzungu barabara hizo zipo  katika hali nzuri kwa wastani wa asilimia 57.80.

Hata hivyo  Nyamzungu amesema kilometa   3,015.59 za mtandao wa Barabara zilizosalia sawa na  asilimia 42.20 hupitika kikamilifu  wakati wa kiangazi tu.

Amesema Serikali kupitia TARURA inaendelea na juhudi ili kuufanya mtandao wote wa Barabara kupitika kwa misimu yote ya Mwaka mkoani Ruvuma.

“Katika mwaka wa fedha 2021/2022 kupitia TARURA Mkoa wa Ruvuma ulitengewa  zaidi ya shilingi bilioni 24, katika bajeti hiyo, TARURA  iliingia mikataba 75 na Wakandarasi ili kuufanya mtandao wa barabara kupitika mwaka mzima’’,alisisitiza.

Mhandisi Nyamzungu amesema katika mikataba hiyo zaidi ya shilingi bilioni 19  zilitengwa kwa ajili ya kutekeleza kazi mbalimbali za matengenezo ya barabara, ujenzi wa madaraja pamoja na makalavati.

Hata hivyo amesema Hadi kufikia Juni,2022 mikataba 70 ya Mfuko wa fedha za Barabara, Jimbo na Tozo ilikamilika kwa asilimia 100 ambapo  mikataba mitano ilivuka mwaka na ipo katika hatua za mwisho za umaliziaji.

Akizungumzia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kupitia fedha za mapato ya ndani   kwa ushuru na maegesho katika kipindi cha  mwaka wa fedha 2022/2023,Mhandisi Nyamzungu amesema, yamefanyika maboresho ya barabara ya Mjimwema Halmashauri ya Mji wa Mbinga yenye urefu wa kilometa 1.1 kwa kiwango cha lami iliyogharimu zaidi ya shilingi milioni 497.

 Ameongeza kuwa TARURA Mkoa wa Ruvuma kwa mwaka huu wa fedha inatekeleza miradi 16 ya maendeleo inayogharimu zaidi ya shilingi bilioni 14 na kwamba miradi hiyo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Hata hivyo amesema kati ya miradi hiyo kupitia Fedha za Mfuko wa Jimbo inatekelezwa Miradi mitano  na  kupitia tozo  inatekelezwa miradi 11.

Amesema Serikali Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kupitia TARURA Mkoa wa Ruvuma imetoa shilingi milioni 750 kwa lengo la kufanya Matengenezo ya barabara ya Luhindo-Mpepo hadi Darpori katika Halmashauri ya Nyasa.

Amesema matengenezo hayo yanahusisha Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha Changarawe na madaraja na kwamba hatua za utekelezaji wa mradi huo zipo katika hatua za umaliziaji.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

 

   

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.