• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TARURA Ruvuma ilivyodhamiria kuweka uwekezaji mkubwa wa miundombinu

Imewekwa kuanzia tarehe: March 30th, 2025

Katika jitihada za kuboresha miundombinu ya barabara, Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoa wa Ruvuma umeidhinishiwa jumla ya Shilingi Bilioni 38.29 kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Meneja wa TARURA Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Silivester Chinengo anasema fedha hizo zinatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika sekta ya usafirishaji, kuboresha maisha ya wakazi wa mkoa wa Ruvuma na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kupitia miundombinu bora ya barabara.

Ufadhili wa Miradi na Matumizi Yake

Kati ya kiasi hicho cha fedha kilichoidhinishwa, Shilingi Bilioni 22.19 zinatoka katika Mfuko wa Barabara (Road Fund), Mfuko wa Jimbo pamoja na Tozo ya Mafuta.

Kulingana na Meneja huyo wa TARURA Mkoa,fedha hizo zitatumika kujenga na kukarabati jumla ya kilometa 1,264.68 za barabara, ambapo kazi zitakazofanyika ni pamoja na Kilometa 6.85 za barabara za lami,Kilometa 398.86 za barabara za changarawe,Kilometa 858.97 za uchongaji barabara,Ujenzi wa madaraja 49,Ujenzi wa makaravati 57 na Ujenzi wa mitaro yenye urefu wa mita 2,610

Mbali na fedha hizi, TARURA Ruvuma pia imepokea Shilingi Bilioni 16.20 kutoka kwa wafadhili wa Umoja wa Ulaya kupitia mradi wa Agri-Connect.

Fedha hizo zinatumika kujenga barabara ya Utiri – Mahande yenye urefu wa kilometa 14.41 kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Mbinga. Mradi huu ni sehemu ya jitihada za kuboresha miundombinu ya barabara ili kusaidia sekta ya kilimo na uchukuzi wa mazao, jambo linalosaidia kuinua uchumi wa wakazi wa eneo hilo.

Faida za Uboreshaji wa Barabara

Utekelezaji wa miradi hii unatarajiwa kuleta manufaa makubwa kwa wakazi wa Ruvuma. Barabara bora zitapunguza gharama za usafiri, kurahisisha usafirishaji wa bidhaa na mazao ya kilimo, na pia kuchochea maendeleo ya biashara katika maeneo mbalimbali.

Aidha, ujenzi wa madaraja na makaravati utawezesha wananchi kusafiri kwa urahisi hata wakati wa mvua kubwa, hivyo kuimarisha usalama wa barabara na usafirishaji.

TARURA Ruvuma imejipanga kuhakikisha kuwa fedha zilizotengwa zinatumika ipasavyo katika kuboresha miundombinu ya barabara.

 Kupitia uwekezaji huu mkubwa, wakazi wa Ruvuma wanatarajia kuona mabadiliko chanya katika sekta ya usafirishaji, hali itakayokuza uchumi na kuboresha maisha ya wananchi kwa ujumla.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.