• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TARURA yatumia bilioni nne kuboresha barabara Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: March 5th, 2023

WAKALA wa barabara za vijijini na mijini (TARURA) wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma, imepokea zaidi ya shilingi Bilioni nne kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na 2022/2023 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya barabara wilayani humo.

Hayo yamesemwa na Meneja wa TARURA wilayani Namtumbo Mhandisi Fabian Lugalaba,wakati akitoa taarifa ya hali ya matengenezo na maboresha miundombinu ya mtandao wa barabara na kueleza kuwa,fedha hizo zimewezesha kufungua mtandao wa barabara maeneo yasiyofikika kiurahisi na ujenzi wa madaraja.

Lugalaba alisema,kati ya fedha hizo shilingi bilioni 2.684  zilipokelewa na kutumika kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kwa ajili ya matengenezo ya barabara zenye urefu wa km 133.62.

Kwa mujibu wa Lugalaba,barabara zenye urefu wa kilomita 103 zilikuwa ni matengenezo ya kawaida na kilomita 30  barabara kwa kiwango cha changarawe.

Aidha alisema,kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Tarura itatumia jumla ya shilingi bilioni 1.409 kufungua barabara mpya kilomita 24,kujenga barabara za lami kilomita 1.6 kufanya matengenezo kwa kiwango cha changarawe kilomita 10 kufanya ukarabati wa kawaida kilomita 161 na kujenga makalavati 4.

Lugalaba alitaja vyanzo vya fedha hizo ni kutoka mfuko wa matengenezo ya barabara,fedha za maendeleo kutoka mfuko wa barabara,fedha za nyongeza  ya tozo kwenye mafuta na fedha kutoka mfuko mkuu wa serikali(jimbo).

Baadhi ya wananchi wilayani humo,wameipongeza serikali kwa kusimamia matengenezo ya barabara ambazo zimesaidia kuboresha na kurahisisha mawasiliano kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Aden Nchimbi alisema,katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan serikali kupitia Tarura,imefanya kazi kubwa ya kufungua na kutengenezo barabara ambazo zimesukuma maendeleo na kuchochea kukua kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja na wilaya ya Namtumbo.

Said Ngonyani mkazi wa Minazini wilayani humo,amewapongeza watumishi wote wa Tarura kwa matumizi sahihi ya fedha zinazotolewa na serikali na usimamizi makini wa miradi ya barabara katika maeneo mbalimbali ambao umesaidia kuifungua wilaya hiyo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.