• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TEMESA Ruvuma walivyodhamiria kuboresha huduma kwa wateja

Imewekwa kuanzia tarehe: January 23rd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas  amewapongeza Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) mkoani Ruvuma kwa kufanya maboresho mbalimbali ya utoaji huduma kwa wateja.

Kanali Thomas ametoa pongezi hizo wakati anafungua kikao cha wadau wa TEMESA kutoka wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma kilichofanyika kwenye ukumbi wa  Chandamali mjini Songea.

Amesema kwa muda mrefu wadau wa TEMESA walikuwa na malalamiko kadhaa kuhusu huduma zisizoridhisha ikiwemo gharama kubwa za matengenezo,matengenezo kuchukua muda mrefu,matengenezo kujirudia,upungufu wa watumishi,kuchakaa kwa miundombinu na uhaba wa vitendea kazi.

“Mtendaji Mkuu wa TEMESA  ameyataja maboresho mbalimbali ambayo yanatarajia kufanywa ili kuboresha huduma ikiwemo kuingia mikataba na wazabuni wa vipuri na vilainishi ili kupunguza muda wa ununuzi’’,alisisitiza RC Thomas.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa ameipongeza serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za kukarabati karakana na kununua vitendea kazi katika karakana ya TEMESA mkoani Ruvuma hali ambayo amesema itaongeza ufanisi katika kazi.

Amesisitiza kuwa  mikakati na maboresho  yanayoendelea yakisimamiwa vizuri huduma inayotolewa na TEMESA itakuwa bora na rafiki kwa wadau.

Awali Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa TEMESA ambaye pia ni Mkurugenzi wa Matengenezo na Huduma za Ufundi Mhandisi Hassan Karonda  amesema Serikali imesaidia kufanya maboresho makubwa yanayoonekana katika Taasisi ya TEMESA.

Ameyataja baadhi ya maboresho yanayoendelea ni kukarabati ofisi za TEMESA katika mikoa ya Ruvuma,Mbeya,Arusha,Mwanza,Dodoma ,Tanga,Morogoro,Lindi,Mtwara,Mara,Kigoma,Tabora na Kagera.

 Maboresho mengine ameyataja kuwa ni ununuzi wa vivuko vipya na kununua vitendea kazi hali ambayo imetatua changamoto kubwa zilizokuwa zinaikabili TEMESA na kwamba mwaka huu imetengwa bajeti ya zaidi ya shilingi 700 kwa ajili ya kununua vitendea kazi vya kisasa.

Naye Mkurugenzi wa Huduma Saidizi wa TEMESA Josephine matiro amesema serikali imedhamiria kuboresha huduma zinazotolewa na TEMESA kwa lengo ya kutoa huduma bora na zenye viwango kwa wateja wao.

Amesema TEMESA ameamua kufanya vikao ya wadau wake kutoka mikoa yote 26 ili kupata maoni ya wadau inayowahudumia ili kutoa huduma zenye tija .

Mmoja wa wadau wakizungumza kwenye kikao hicho Wakili Julius Mtatiro ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tunduru ametoa rai kwa   watendaji wa TEMESA nchini kuweka mikakati ya kuwafikia  wadau wote badala ya kutegemea Taasisi za serikali.

Amesema watu binafsi sasa wanaweza Kwenda kutengeneza  magari yao TEMESA baada ya maboresho makubwa yaliyofanywa  hivyo kuvutia wateja wengi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.