• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TUNDURU walivyojipanga kukabiliana na ugonjwa wa MPOX

Imewekwa kuanzia tarehe: March 29th, 2025

Kikao muhimu cha kujadili mikakati ya tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Mpox kimefanyika wilayani Tunduru, mkoani Ruvuma kikiwakutanisha viongozi wa serikali, wataalamu wa afya, na wadau mbalimbali wa sekta ya afya. 

Kikao hicho kililenga kuhakikisha wilaya inakuwa tayari kukabiliana na ugonjwa huo iwapo utaripotiwa katika eneo hilo.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Tunduru, Ndugu Milongo Sanga, aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya, Mheshimiwa Simon Chacha, aliwataka wananchi kutohofia ugonjwa wa Mpox kwani hadi sasa hakuna mgonjwa aliyeripotiwa wilayani humo. 

Alihimiza wananchi kufuata maelekezo ya wataalamu wa afya na kuchukua tahadhari zinazostahili ili kuzuia maambukizi.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya, Bi. Grace  Mhagama, aliwataka washiriki wa kikao hicho kuwa mabalozi wa afya kwa jamii, akisisitiza kuwa kila mtu ana jukumu la kueneza elimu kuhusu dalili, njia za maambukizi, na namna ya kujikinga na Mpox. 

Alibainisha kuwa uelewa wa jamii utasaidia kudhibiti ugonjwa huo mapema.

Mganga Mfawidhi wa Wilaya hiyo Dr.Athumani Mkonoumo, aliwaeleza washiriki kuwa Mpox hauna tiba ya moja kwa moja, lakini wagonjwa hupatiwa matibabu ya kupunguza dalili. 

Alielezea umuhimu wa utengaji wa wagonjwa ili kuzuia maambukizi zaidi na kusisitiza kuwa ufuatiliaji wa karibu wa visa vyovyote vinavyoshukiwa ni muhimu.

Afisa Afya wa Wilaya, Bwana Ayubu Majumbewima, alielezea hatua zinazochukuliwa na halmashauri katika kuelimisha jamii kuhusu Mpox

Alisema kampeni za uhamasishaji zinaendelea kupitia kliniki, mashule, mikutano ya hadhara, na vyombo vya habari na kwamba hospitali ya wilaya imetenga jengo maalum kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa watakaobainika na ugonjwa huo, huku usafiri wa dharura ukiwa tayari kwa ajili ya wagonjwa na wataalamu wa afya.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.