• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TUNDURU wataka wawekezaji wenye tija sekta ya utalii

Imewekwa kuanzia tarehe: June 15th, 2022

WAKATI mchakato wa kumpata mwekezaji katika Jumuiya ya Uhifadhi  Wanyamapori Nalika wilaya yaTunduru mkoani Ruvuma ukitarajiwa kukamilika wiki ijayo,baadhi ya Wananchi wa kijiji cha Rahaleo na Mbungulaji kata ya Kalulu wameiomba Bodi ya  ushauri wa maliasili ya wilaya hiyo na Serikali kupitia wizara ya Maliasili na Utalii kuchagua mwekezaji mwenye sifa atakayesaidia kukuza sekta ya utalii  na kulipa kodi za Serikali na kushirikiana na jamii.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao wakiongozwa na Diwani wa kata ya Kalulu Mbale Motamota wamesema,wilaya ya Tunduru inazungukwa na Hifadhi ya Taifa ya Nyerere pamoja na Jumuiya mbalimbali za Wanyamapori ikiwamo ya Jumuiya ya Hifadhi   ya Nalika ambayo  katika kipindi cha miaka mitano imeongoza kutembelewa na idadi  kubwa ya watalii wanaoingia katika wilaya hiyo.

Said Pachana mkazi wa Rahaleo alisema,kwa miaka mingi hawakuwa na mwekezaji,lakini ilipofika mwaka 2017 walipata mwekezaji mmoja kampuni ya Best Luxury Safaris ambaye aliwezesha utalii  kukua japo kwa ugumu kutokana na hali mbaya ya miundombinu ya kitalu.

Alisema,mwekezaji huyo amefanya kazi nzuri  ya kuwafikisha  apa walipo na wanaamini kama wataendelea kushirikiana naye wanaweza kuwa mfano mzuri kwa wana Kusini na Tanzania kwa ujumla katika suala zima la uwekezaji katika sekta ya utalii.

Pachana,ameiomba bodi  ya ushauri wa mambo ya maliasili ngazi ya wilaya,jumuiya ya Nalika na kamati ya mchakato wa kumpata mwekezaji kutowapa nafasi watu watakaorudisha nyuma juhudi zinazofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan za kukuza na kuendeleza sekta  hiyo hapa nchini.

Sharifu Galimbe mkazi wa Rahaleo, ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa jitihada zake za kuboresha sekta  hiyo,hata hivyo ameishauri kuwa makini na baadhi ya watu wanaoomba  kuwekeza katika Jumuiya ya Wanyamapori ya Nalika.

Alisema,kama itashindikana kumpata mtu mwenye sifa, basi ni vyema kumpa nafasi hiyo mwekezaji wa awali Kampuni ya Best Luxury Safaris ambaye ameonesha  uwezo  mkubwa wa kuendeleza  utalii na kuchangia uchumi wa Tunduru.

Mkazi wa kijiji cha Milonde Said Mbalamahengo alisema,kwa muda mrefu hawajawahi kuona wageni wakifika kwenye vitalu vya uwindaji vilivyo chini ya Jumuiya hiyo,lakini baada ya Kampuni ya Best Luxury Safaris kuanza  shughuli zake wameshuhudia wageni wengi wa ndani na nje ya Tanzania wanaofika kutembelea vitalu hivyo vya utalii wa uwindaji.

Ameiomba Bodi hiyo, kutowapa nafasi wawekezaji wenye Historia mbaya na wababaishaji  bali wahakikishe wanampata mwekezaji kama alivyo Kampuni ya Best Luxury Safaris ambaye katika kipindi cha miaka mitano ametoa mchango mkubwa katika sekta ya utalii na kuchangia maendeleo kwa vijiji vinavyounda Jumuiya ya Uhifadhi wa Wanyamapori Nalika.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Nalika Said Masoud alisema,jumla ya makampuni manne yamejitokeza kuomba kuwekeza utalii wa uwindaji baada ya mwekezaji  wa mwanzo muda wake kumalizika.

Alisema, katika mchakato huo wataangalia kumpata mwekezaji  ambaye atalipa vizuri mapato ya Serikali, ya jumuiya na kusaidia shughuli za maendeleo kwenye vijiji vinavyounda jumuiya hiyo.

Ameipongeza Kampuni ya Best Luxury Safaris kwa kuchangia maendeleo katika vijiji mbalimbali na kuyataka  makampuni mengine ya uwekezaji katika sekta ya utalii kuiga utendaji nzuri na ushirikiano mkubwa kwa jamii.

Alisema, katika kipindi  kifupi imetoa mchango mkubwa katika shughuli na ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwamo katika sekta ya afya na elimu katika wilaya hiyo.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Kalulu Mbale Motamota alisema,kwa sasa wapo mahali pazuri ikilinganisha na walipotoka,lakini ameonesha wasiwasi wake juu ya mchakato wa kumpata mwekezaji mpya ambaye anaweza kurudisha nyuma juhudi kubwa zilizoanza kufanywa na Serikali ya awamu ya sita kuimarisha sekta ya utalii.

Motamota alisema,katika mchakato huo unaotarajiwa kuhitimisha wiki ijayo kuna waombaji ambao hawafai  kutolea mfano Kampuni ya Safari Shallom inayomilikiwa na mtu aliyemtaja kwa jina la Ryan Shallom ambaye amewahi kuwa mwekezaji katika vitalu mbalimbali hapa nchini,lakini Histori ya uwekezaji wake ni mbaya.

Alisema, mwaka 2021 amewahi kuwa mmoja wa wasimamizi wa kambi za uwindaji wa kitalii za Kampuni ya Best Luxury Safaris ambayo ilikuwa mwekezaji wao na yeye kama msimamizi alifanya mambo mengi mabaya  ikiwamo kutolipa fedha za wafanyakazi,kuuwa wanyama bila vibali na kugawa nyama hizo kwa wananchi kama rushwa ili wamsaidie kukubalika kuwa mwekezaji mpya.

Aidha alisema,Shallom amehusika kutoa rushwa za fedha kwa baadhi ya viongozi wa Jumuiya na vijiji, hali iliyopelekea kukamatwa na  maafisa waTaasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa(Takukuru)wilayani Tunduru.

“nimewahi kupokea malalamiko  ya wananchi  wapatao 25 kutoka kwenye vijiji vinavyounda Jumuiya ya Nalika wakilalamikia  kutolipwa mishahara yao na walikuwa wanajiandaa kwenda kudai haki zao kwa nguvu,jambo ambalo lilikuwa linakwenda kuleta uvunjifu wa Amani”alisema.

Aliongeza kuwa,kama Diwani alijaribu kutatua tatizo hilo bila mafanikio kutokana na usumbufu wake hadi alipoomba msaada  kwa Mkuu wa wilaya ya Tunduru ambaye alisaidia kumaliza tatizo hilo.

Motamota,ameiomba Serikali,bodi ya ushauri ya mambo ya maliasili wilaya,Jumuiya ya Nalika pamoja na  kamati ya mchakato wa kupatikana kwa mwekezaji mpya waepuke kuwaleta wawekeza wenye sifa hizo ambao watasababisha matatizo na migogoro mikubwa kwa jamii na serikali.

“naomba sana bodi ya ushauri,jumuiya ya Nalika wafanye uchambuzi wa kina ili watupatie mwekezaji bora atakayefanya utalii wetu uendelee badala ya kutuingiza kwenye migogoro na kuua utalii wetu  unaokuwa kwa changamoto nyingi”alisema Motamota.

Alipotafutwa Shallom ili kutoa ufafanuzi wa  tuhuma hizo hakuweza kupatikana kwa kuwa anaishi mkoani Mororogoro, na hata alipotafutwa kwa simu ya mkononi hakuweza kupatikana kwa kuwa simu zake zinashikiliwa na Takukuru kwa ajili ya uchunguzi.

Hata hivyo gazeti hili lilimtafuta Wakili wa Shallom,  Wakili Ismail Kaukuya ambaye naye alidai mteja wake hapatikani kwenye simu yake ya mkononi na kwamba anaendelea kumtafuta kwa mawasiliano zaidi.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.