• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TUNDURU yapokea bilioni 1.22 kupitia BOOST kuboresha miundombinu ya elimu ya msingi

Imewekwa kuanzia tarehe: May 30th, 2023

WILAYA ya Tunduru mkoani,imepokea jumla ya Sh.bilioni 1,224,600,000.00 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kuboresha upatikanaji wa fursa sawa katika ujifunzaji bora kwa elimu ya awali na msingi Tanzania Bara(Boost).

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya hiyo Julius Mtatiro,wakati akizindua ujenzi wa  vyumba tisa vya madarasa katika shule ya msingi Tinginya kata ya Tinginya vinavyojengwa chini ya mradi huo maalum.

Alisema,fedha hizo zitatumika kujenga ofisi za walimu,matundu ya vyoo,vichomea taka na madawati na kumaliza kabisa changamoto ya miundombinu kwenye shule za msingi wilayani Tunduru ambazo nyingi zimejengwa miaka ya zamani.

Alisema,shule hizo zitakuwa za mfano kutokana na ubora wake na kumshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu ya awali na msingi wilayani humo.

Kwa mujibu wa Dc Mtatiro ni kwamba Serikali  ya awamu ya sita  imeanza kuboresha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia katika shule zote za umma ili ziwe bora na rafiki kwa wanafunzi na walimu.

Mtatiro,amehaidi kusimamia matumizi  ya fedha zote na atahakikisha miundombinu inajengwa kwa ubora wa hali ya juu ili ilingana na thamani halisi ya fedha zilizotolewa na kuwaonya wasimamizi na watekelezaji wa miradi kutothubutu kuchezea fedha wala vifaa vitakavyoletwa kwa ajili ya kazi.

Pia alisema,ameagiza miradi yote itakayotekelezwa katika wilaya hiyo  kwa njia ya force akaunti ifanywe na mafundi kutoka eneo husika na kazi za kufyatua tofali zifanywe na vijana wa jeshi la akiba(mgambo), badala ya kuwatafuta watu kutoka nje ya Tunduru.

Alisema,hatua hiyo itasaidia sana miradi inayojengwa kulindwa kwa kuwa wananchi wataiona ni yao na hivyo kusimamiwa kwa karibu na jamii itafaidika na uwepo wa miradi hiyo kwa kufanya kazi za kuwaingizia kipato.

Katika hatua nyingine,Mtatiro amewaasa  wananchi hasa vijana kutokubali kurubuniwa na baadhi ya watu wasiokuwa na nia njema na serikali kwa kuwashawishi kukataa kushiriki na kufanya kazi za kujitolea katika maeneo yao.

Amewataka wananchi wa Tinginya na vijiji  vingine wilayani humo, kuwa wavumilivu na kuendelea kushirikiana na serikali iliyopo madarakani katika ujenzi wa miradi ya maendeleo yenye lengo la kuboresha huduma mbalimbali za kijamii.

Kwa upande wake mratibu elimu kata ya Tinginya Rashid Chalamanda alisema,wamepokea kiasi cha Sh.milioni 331,600,000 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa tisa kati ya hayo mawili kwa ajili ya elimu ya awali,matundu ya choo,jengo la utawala na kichomea taka.

Alisema,ujenzi wa madarasa hayo utasaidia sana kumaliza changamoto ya mlundikano wa watoto madarasani na kushawishi kupenda shule na hivyo wilaya hiyo kupiga hatua kielimu kama ilivyo katika maeneo mengine hapa nchini.

Diwani wa kata ya Tinginya Eliasa Pelemende alisema,wananchi wa kata hiyo wako tayari kushiriki na kujitolea nguvu zao katika ujenzi  huo ili kazi ikamilike haraka.

Mwanafunzi wa darasa la nne katika shule ya Tinginya Maliche Mohamed,ameishukuru Serikali kuwajengea vyumba vipya  vya madarasa ambavyo vitamaliza kero ya kukaa wanafunzi wengi katika chumba kimoja.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.