• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UJENZI wa bandari ya Mbambabay waanza

Imewekwa kuanzia tarehe: February 27th, 2024

SERIKALI imeanza ujenzi wa Bandari mpya na ya kisasa katika mji wa mdogo wa Mbambabay wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma,itakayokuwa makao makuu ya bandari zote za ziwa Nyasa ambayo itaunganisha nchi za Malawi na Msumbiji.

Meneja wa Bandari za Ziwa Nyasa Manga Gassayah alisema, ujenzi wa bandari hiyo ni mkakati wa serikali ya awamu ya sita kuimarisha ushoroba wa maendeleo wa Mtwara(Mtwara Development Corridor) ambayo ni njia fupi na rahisi ya kuhudumia mizigo ya nchi jirani za Malawi kutoka Bandari ya Mtwara.

Alisema,mradi huo utahusisha ujenzi wa gati lenye uwezo wa kuhudumia meli mbili,jengo la utawala la ghorofa tatu,jengo la abiria,barabara ya kuingia bandarini,majengo ya kuhifadhi shehena za mizigo na unatekelezwa na kampuni ya Xiamen Ongoing Group Co Ltd ya nchini China kwa gharama ya Sh.bilioni 81.

Alisema,wa bandari hiyo utakamilika kwa muda wa miezi 24(miaka 2) ambapo itaongeza uwezo wa kuhudumia shehena ya mizigo kwa bandari za ziwa Nyasa kutoka tani 110,000 za sasa hadi tani 550,000 kwa mwaka.

Gassayah alitaja manufaa ya mradi huo mara utakapokamilika ni pamoja na kuongeza uwezo wa bandari kupokea meli kubwa na kuhudumia mizigo kwa wingi na kuwa kiungo muhimu kwa sekta ya usafiri na usafirishaji kati ya bahari ya Hindi na ziwa Nyasa.

Kwa mujibu wa Gassayah,faida nyingine zitakazopatikana ni kukuza viwanda vidogo na vya kati na kuongeza mauzo na uagizaji wa bidhaa nje ya nchi,kuongeza pato la mwananchi na serikali,kuboresha usalama wa vyombo vya abiria na kutoa ajira na biashara wakati wa ujenzi na wakati wa uendeshaji.

Pia alisema,serikali kupitia mamlaka ya bandari nchini(TPA)imepanga kujenga gati ndogo kwenye baadhi ya bandari ikiwemo bandari ya Liuli katika wilaya ya Nyasa,Manda wilaya ya Ludewa mkoani Njombe,Matema na Kiwira katika wilaya ya Kyela mkoani Mbeya.

Alieleza kuwa,miradi hiyo imepangwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2023/2024 na tayari serikali imeshatoa fedha jumla ya Sh.bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa miradi hiyo muhimu kwa uchumi wa nchi.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa uchukuzi David Kihenzie,amemtaka mkandarasi anayejenga bandari hiyo kuhakikisha anazingatia ubora na muda uliopangwa ili wananchi waweze kuitumia katika shughuli zao za kujiletea maendeleo.

Alisema,mradi huo ni wa kihistoria na ni mapenzi na maono makubwa ya Rais wetu Dkt Samia Suluhu Hassan kwa wananchi wa Nyasa na mkoa wa Ruvuma.

Kihenzie,amewataka wananchi hususani vijana kuchangamkia fursa ya ujenzi wa bandari hiyo kwa kufanya kazi zitakaowaingizia kipato,kuwa walinzi wa vifaa vitakavyoletwa kwa ajili ya ujenzi na kuhaidi kuwa mradi huo utakamilika kwa muda uliopangwa.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri alieleza kuwa,serikali ya awamu ya sita imeanza mchakato wa ujenzi wa Reli kutoka Mtwara-hadi Mbambabay mkoani Ruvuma ili kutoa fursa kwa wafanya biashara kusafirisha bidhaa na mizigo kwenda nchi jirani ya Msumbuji na Malawi kupitia ziwa Nyasa.

Mbunge wa jimbo la Nyasa Stella Manyanya, ameishukuru serikali kutoa fedha zitakazotumika kujenga bandari mpya katika mji pekee wa kitalii wa Mbambabay wilayani Nyasa ambayo itasaidia sana kuharakikisha kukua kwa Uchumi wa mtu mmoja mmoja,wilaya na mkoa wa Ruvuma.

Mkazi wa mji wa Mbambabay Ramadhan Mkilinya,ameiomba serikali kupitia mamlaka ya bandari nchini (TPA) kuhakikisha vijana wa Nyasa wanapewa kipaumbele katika ujenzi wa bandari hiyo badala ya kutafutwa watu kutoka nje ya Nyasa na mkoa wa Ruvuma.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.