• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UJENZI wa barabara ya mchepuko Songea kuanza karibuni

Imewekwa kuanzia tarehe: October 3rd, 2022

WAKALA wa Barabara Tanzania(TANROADS) Mkoa wa Ruvuma, iko katika hatua ya mwisho kuanza  ujenzi wa Barabara ya  mchepuko( Songea ByPass)maarufu kama (Mtwara Corridor)yenye urefu wa km 14.3.

Meneja wa TANROADS mkoani Ruvuma Mhandisi Ephatar Mlavi alisema,barabara hiyo ni sehemu ya ujenzi wa mradi wa Barabara kuu ya Songea-Makambako.

Kwa mujibu wa Mhandisi Mlavi ni kwamba,ujenzi wa Barabara hiyo itaanzia eneo la Namanditi ambapo itapita kata ya Mwenge msindo,Msamala, kituo cha kupoza umeme  Unangwa hadi  Changarawe Barabara kuu ya Songea-Tunduru.

Aidha alisema,katika mradi huo kutakuwa na eneo la mzunguko (round about) tatu  ya kwanza itejengwa eneo la Namanditi,ya pili Msamala karibu na kituo cha mafuta cha Ottawa na nyingine itajengwa eneo la Changarawe Barabara kuu ya Songea-Tunduru.

Alisema, pindi Barabara hiyo itakapojengwa itasaidia sana kuondoa changamoto ya msongamano wa magari katikati ya mji wa Songea hasa malori yanayobeba makaa ya mawe na itakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi.

“Barabara  hii ya mchepuko(Songea Bypass) ina umuhimu mkubwa na itaongeza fursa nyingi  za kiuchumi kwa wakazi  wa mkoa wa Ruvuma  na wale wanaofika kutoka mikoa mingine ya  jirani”alisema Mlavi.

Kwa mujibu wa Mlavi, tathimini ya fidia kwa ajili ya kuwalipa wananchi  watakaopitiwa na  mradi huo imeshafanyika  na sasa Serikali iko katika hatua ya mwisho ya malipo ili wananchi waweze kupisha ujenzi wa mradi huo.

Mhandisi Mlavi, amewataka wananchi wa mkoa wa Ruvuma na Watanzania kwa ujumla kuiamini Serikali yao kwani imejipanga vyema kwa ajili ya kutekeleza mradi huo na miradi mingine katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Ruvuma.

“nachukua nafasi hii kuwatoa wasiwasi wananchi kuhusu ujenzi wa Barabara hii kwani serikali iko kazini na imejipanga kuhakikisha  itajengwa kwa kama ilivyokusudia”alisema Mlavi.

Naye Mhandisi Izaki Issa kutoka ofisi ya meneja wakala wa Barabara Tanzania(TANROADS)mkoa wa Ruvuma alisema, Barabara  hiyo ya mchepuko itapita katika vijiji vitano vya Namanditi,Luwawasi,Mtaungana,Osterbay na Kuchile.

Baadhi ya wananchi,wameiomba Serikali kuanza ujenzi wa Barabara hiyo  haraka ili iweze kuchochea ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Ruvuma na kuharakisha maendeleo yao.

Mariam Mwela mkazi wa Namanditi alisema, wameupokea mradi huo kwa mikono miwili kutokana na faida zake kiuchumi  na ameipongeza TANROADS mkoa wa Ruvuma kufikiria kujenga Barabara  ya mchepuko katika mji wa Songea.

Aidha,ameiomba Serikali kuwalipa fidia zao mapema ili wakatafute maeneo mengine  ya kuishi,kwani tangu TANROADS ilipoweka alama za X kwenye nyumba zao wanashindwa kuendeleza maeneo yao na wanaishi kwa hofu kubwa.

Pascal Msigwa(Top One)alisema,mradi huo ni muhimu sana kwa wananchi wa mkoa wa Ruvuma na kuipongea serikali ya awamu ya sita kwa kuonyesha nia ya kujenga  Barabara hiyo na  Barabara kuu ya Songea-Makambako.

Rajabu Kanganya mwendesha boda boda, ameiomba Serikali kupitia TANROADS mkoa wa Ruvuma,kuhakikisha mradi huo unaanza haraka badala ya kuchukua muda mrefu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.