• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

USHAMILI wa homa ya ini wapungua nchini

Imewekwa kuanzia tarehe: July 29th, 2025

Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama, amesema viashiria vya ushamili wa homa ya ini vinaonyesha kuwa umeshuka nchini kwa takwimu za utafiti wa homa ya UKIMWI za mwaka 2022/23 ukilinganisha na takwimu za mwaka 2016/17.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama, wakati akitoa tamko la wizara katika maadhimisho ya siku ya homa ya ini duniani, ambapo ametoa tamko hilo mkoani Ruvuma.

“Kulingana na takwimu za utafiti wa homa ya UKIMWI kwa mwaka 2022/23 ni asilimia 3.5 kwa homa ya ini inayosababishwa na virusi vya aina ya B, na asilimia 0.2 inavyosababishwa na aina ya C, viashiria vyote vinaonyesha ushamili huo umeshuka kutoka takwimu za utafiti wa hali ya UKIMWI kwa mwaka 2016/17 ambapo ilikuwa ni asilimia 4.0 kwa homa ya ini uambukizo wa virusi vya aina ya B na asilimia 1 inayoambukizwa kwa virusi vya aina ya C,” alisema Mhagama.

Chanjo ya homa ya ini aina ya B hutolewa bila malipo kwa watoto wachanga, huku watu wazima wakichangia kiasi kidogo, hivyo amewataka wananchi kujitokeza kupima viashiria vya ugonjwa ya homa ya ini katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amesema kuwa takwimu za kitaifa za mwaka 2022/2023 zinaonyesha kuwa asilimia 2.0 ya watu wenye umri wa kuanzia miaka 15 wameambukizwa virusi vya homa ya ini, sawa na watu wawili kati ya kila watu 100.

Amebainisha kuwa mkoa wa Ruvuma una zaidi ya watu 24,000 waliothibitishwa kuwa na homa ya ini, ambapo wanaume ni takribani 17,000 na wanawake 7,000.

Maadhimisho ya Siku ya Homa ya Ini Duniani hufanyika kila mwaka tarehe 28 Julai, yakilenga kuongeza uelewa kuhusu ugonjwa huu hatari na kuchochea hatua za kudhibiti maambukizi. Kwa mwaka 2025, kauli mbiu ni: "Ondoa Vikwazo, Tokomeza Homa ya Ini", ikisisitiza umuhimu wa kuondoa changamoto zinazozuia watu kupata elimu sahihi, huduma za afya, na chanjo dhidi ya ugonjwa huo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KARIBU RAIS Samia Ruvuma Julai 30,2025

    July 29, 2025
  • USHAMILI wa homa ya ini wapungua nchini

    July 29, 2025
  • NAMTUMBO inavyoandika historia ya madini

    July 29, 2025
  • HOMA ya ini yapungua Tanzania,serikali yaanika mafanikio,yabainisha mkakati mpya kufikia 2030

    July 29, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.