• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

UWANJA wa ndege wa Songea wafunguliwa,ndege kubwa kuanza kutua mwezi ujao

Imewekwa kuanzia tarehe: July 9th, 2020

UWANJA wa ndege wa Songea umefunguliwa baada ya kukamilika ujenzi wake kwa asilimia 50 na ndege kubwa aina ya Bombadier zinatarajia kuanza kutua Agosti mwaka huu.

Akitoa taarifa ya ukarabati wa uwanja huo kwa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma,Mhandisi Mshauri ujenzi wa uwanja wa Songea, Jofrey Keneth amesema wamefikia hatua nzuri ya ujenzi wa uwanja huo hivyo kuruhusu ndege kuanza kutua.

“Hivi sasa ndege ndogo zinatua kwenye uwanja mpya ambao umefunguliwa,uwanja umejengwa kwa mita 800 na Mkandarasi  ataongeza mita nyingine  400 ambazo zitaleta jumla ya mita 1200 hivyo kuwezesha kuruka na kutua ndege kubwa aina ya bombadier’’,alisema.

Amesema Mkandarasi ameahidi kwamba hadi kufika mwishoni mwa mwezi Agosti mwaka huu atakuwa ametimiza kujenga uwanja kwa mita 1200 ambazo  ndizo hitaji la chini zaidi kuwezesha kutua ndege aina ya bombardier.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa uwanja huo ambao unakarabatiwa na Kampuni ya CHICCO kutoka nchini China,Meneja wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma Lasack Alinanuswe,amesema serikali imetoa kiasi cha shilingi zaidi ya bilioni 39 kutekeleza mradi huo ambao mkataba wake ni miezi 20 inayoishia Desemba 28 mwaka huu.

Amesema mradi huo tangu kuanza kutekelezwa umeweza kutoa ajira kwa wafanyakazi 110  ambao wote ni watanzania kutoka mkoani Ruvuma na wachina saba.

“Mhandisi wa ujenzi huo hivi sasa anafanyakazi usiku na mchana ili aweze kukamilisha kazi hiyo  ndani ya mkataba,Juni 28 mwaka huu tulihamisha shughuli za urukaji wa ndege kutoka upande wa  zamani wa 14 kwenda upande mpya wa 32 kwa hiyo hivi sasa ndege zinatumia uwanja mpya’’,alisema.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi  huo kwa niaba ya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma,Mjumbe wa Halmashauri Kuu  CCM Taifa Musa Homera amesema wakazi wa Ruvuma wanalalamika kupanda ndege kwa gharama kubwa toka Songea hadi Dar es salaam ambapo wanalipa nauli ya shilingi milioni moja kwenda na kurudi.

Amesema nauli ya ndege za serikali ni gharama nafuu  hivyo ni matarajio ya wananchi wa Mkoa wa Ruvuma,kuona sasa Songea inafunguka kupitia usafiri wa anga ambao watu wengi wanaweza kumudu.

“Hivi sasa Songea imejifunga,hatuwezi kupokea wageni toka mbali,watu wanashindwa kusafiri kwa njia ya barabara ambayo ni zaidi ya saa 15 toka Dar es salaam hadi Songea,lakini usafiri wa ndege ukianza watu watanufaika wakiwemo wagonjwa’’,alisisitiza Homera.

Amesema Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Ruvuma,inahimiza uwanja wa ndege wa Songea ufunguliwe sio kwa sababu kupenda anasa bali ni mahitaji ya wananchi wa Mkoa wa Ruvuma na nchi jirani za Msumbiji na Malawi.

Naye Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma Nuru Ngereja amesema Kamati ya Siasa ya CCM ingetamani miradi yote ikamilike kabla ya Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba mwaka huu kwa kuwa serikali iliahidi na imetekeleza.

Uwanja wa ndege wa Songea ulijengwa kati ya mwaka 1974 hadi 1980 umewekewa lami hivyo kuwa na uwezo wa kutua ndege majira yote masika na kiangazi.

Imeandikwa na Albano Midelo                                    

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 9,2020

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.