• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

VIONGOZI wa AMCOS waliojaribu kumhonga Mkuu wa TAKUKURU Tunduru wahukumiwa kifungo

Imewekwa kuanzia tarehe: September 20th, 2024

Viongozi wa Majimaji AMCOS Waliojaribu Kumuhonga Mkuu wa Takukuru Tunduru wahukumiwa kulipa faini  ya Milioni 1.5 na jela Miaka miwili

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya wa Tunduru mkoani Ruvuma imewahukumu viongozi wanne wa vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) kulipa faini ya shilingi milioni 1.5 na kifungo jela miaka miwili.

Viongozi waliohukumiwa ni   Issa Rashid Makopi ambaye ni Mwenyekiti Majimaji AMCOS Tunduru, Mtuva Said Rashid  ambaye ni Meneja Msaidizi Majimaji AMCOS,Mfaume Zuberi Mambo, Meneja Majimaji AMCOS na Halfa Said Chipangula  Meneja Naluwale AMCOS.

Viongozi hao wamehukumiwa  adhabu hiyo kutokana na  kutoa hongo  ya shilingi 800,000/= kwa Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Tunduru George Njogolo ili asiendelee na uchunguzi dhidi yao uliohusu ubadhilifu wa mbolea aina ya salfa inayotolewa bure na Chama Kikuu cha Ushirika Tunduru (TAMCU LTD) kwa wakulima wa korosho waliopaswa kupewa na Viongozi hao kinyume na kifungu cha 15 (1) (b) na(2) vya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa [Sura ya 329 mapitio ya 2022.

Hukumu dhidi ya Viongozi hao ilitolewa Septemba 18,2024 na Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya Tunduru Bw. Shughuli J Mwampashe (SRM) akishirikiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Bw.Mwinyi Yahaya.

Washitakiwa wametiwa hatiani na Mahakama imewahukumu kulipa faini ya Shilingi Milioni 1.5  na kutumikia kifungo cha miaka miwili jela.Pia fedha kiasi cha shilingi 800,000/= kimetaifishwa na kuwa mali ya Serikali  na kimewekwa katika akaunti ya Kamanda Uchunguzi Ruvuma

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.