• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

VITA ya corona,watu 92 Songea wawekwa karantini

Imewekwa kuanzia tarehe: April 29th, 2020

KITUO cha Uhamiaji cha Mkenda kilichopo wilayani Songea mpakani mwa Tanzania na Msumbiji kimeweza kuhudumia  raia wa kigeni na watanzania wapatao 174 katika kipindi cha kuanzia Aprili Mosi hadi 27,2020.

Akitoa taarifa ya kituo hicho  kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme alipofanya ziara ya kutembelea kituo hicho,Afisa Uhamiaji Kituo cha Mkenda Inspekta Ambinga Swai  amesema kati ya wageni waliohudumiwa katika kipindi hicho ni raia wa Tanzania walioingia nchini ni 73,raia wa Tanzania waliotoka nchini ni 44,raia wa kigeni walioingia nchini 17 na raia wa kigeni waliotoka nchini ni 40.

Hata hivyo  Swai amesema raia wa kigeni na watanzania waliotoka nje ya nchi na kuingia nchini walianza kupelekwa katika eneo la karantini lililopo Peramiho nje kidogo ya Mji wa Songea kuanzia Aprili 6 na kwamba hadi kufikia Aprili 27 jumla ya watu 92 walikuwa kwenye karantini.

Amesema kati ya watu hao raia wa Tanzania ni 82 na  raia wa kigeni 10 na kwamba katika idadi ya waliopelekwa karantini kulikuwa na Mkisiwa mmoja ambaye ni raia wa Tanzania.

Akizungumza baada ya kukagua kituo hicho Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ameipongeza Idara ya Uhamiaji kwa ,kazi nzuri na kutahadharisha katika kipindi hiki cha vita ya corona kuchukua tahadhari ambapo amekemea wasishiriki katika vitendo vya rushwa kujaribu kuwapitisha wageni wanaotoka nje ya nchi bila karantini.

Amewashauri kuchukua tahadhari zilizotolewa na watalaam wa afya ikiwemo kunawa mikono,matumizi ya vitakasa mikono na matumizi ya barakoa na kwamba raia wote wanaoingia nchini lazima wawekwe karantini kwa siku 14.

“Wapimeni wageni wote wanaongia nchini awe ni  Mtanzania au raia wa kigeni ,tumewaleta thermal scanner,ugonjwa huu ni hatari,nichukue fursa hii kuwapongeza watumishi wote wa afya ambao wamesimama imara,nakuomba Mganga Mkuu angalia maslahi ya watumishi wa afya’’,alisisitiza.

Amesema kila mmoja akiwajibika na kushirikiana kwa pamoja vita ya corona tutaishinda na kwamba kumuumba Mungu katika janga hili kuende sanjari na juhudi za kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ametoa shilingi 500,000 kama motisha kwa askari watano wanaolinda eneo la mpaka wa Mkenda ili kuhakikisha kuwa nchi na Mkoa wa Ruvuma unaendelea kubaki katika hali ya usalama.

Kituo cha uhamiaji Mkenda chenye Taasisi tano kipo umbali wa kilometa 140 kutoka mjini Songea,kituo hicho ambacho kimepakana  na nchi ya Msumbiji kilianza kufanyakazi tangu mwaka 2009.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma.

Aprili 29,2020

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.