• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WADAU wote wa uchaguzi kupata elimu ya uchaguzi kabla ya Oktoba 28

Imewekwa kuanzia tarehe: October 5th, 2020

KAMISHINA wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu ambae ni k Mary Longway amefungua mkutano wa wadau wa uchaguzi Mkoa wa Ruvuma uliofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

 Akizungumza mbele ya waandishi wa Habari,Wakati wa kufungua mkutano huo Longway amesema Tume ya Taifa kutokana na sheria ya uchaguzi sura ya 343 imepewa mamlaka ya kutoa Elimu ya mpiga kura nchi nzima,kuratibu na kusimamia asasi Zinazotoa Elimu hiyo.

Vilevile, amesisitiza umuhimu ushirikishwaji wa wadau wa uchaguzi kupitia mawakala wa vyama vya siasa, kwa sababu siku ya uchaguzi vyama vya siasa vimepewa nafasi ya kuweka wakala katika Kila kituo cha kupigia kura.

"Tume inawahakikishia wananchi kuwa imejipanga katika kusimamia uchaguzi wa mwaka huu kwa kufuata katiba, sheria, kanuni na miongozo mbalimbali na Tume inaamini kuwa Kila mdau akitimiza wajibu wake kwa kufuata taratibu, watanzania wataweza kupiga kura kwa amani siku ya uchaguzi", amesema Longway.

Kwa upande wake Afisa Uchaguzi Mkoa wa Ruvuma Happy Msanga amesema Tume inawatoa hofu wapiga kura wote wenye mahitaji maalumu kwa kuwa maelekezo yametolewa kwa watendaji wa uchaguzi kutoa kipaumbele kwa watu wanaoishi na ulemavu, wajawazito, akina Mama wanaonyonyesha waliokwenda na watoto vituoni, wazee na wagonjwa.

Amesisitiza kuwa  Tume imewaangalia watu wote  uhitaji maalumu wataweza kupiga kura kutokana na uhitaji wake na kwamba matarajio ya Tume ni kuona Kila mwananchi mwenye sifa ya kupiga kura anajitokeza na kadi yake ya kupiga kura katika kituo alichojiandikisha ili kutimiza haki yake ya msingi ya kikatiba.

 Askofu wa Kanisa la kirutheri Dayosisi ya Mkoa wa Ruvuma Amon Mwenda amesema yeye Kama kiongozi wa dini ni wajibu wake kutoa Elimu ya uchaguzi kwa wananchi kwa sababu ni sehemu ya utume wake kutokana nafasi aliyonayo anakutana na watu mbalimbali kwa muda tofauti.

Naye Mkurugenzi wa Kituo cha Wasaidizi was Sheria ( Songea Paralegal Centre) Fatma Missango amesema wamepewa thamani kubwa sana na Tume ya uchaguzi  kwenda kutoa mafunzo kwa Umma kwa watu wengi ambao hawana uelewa kuhusu uchaguzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza Huru la Wazee Manispaa ya Songea Elzear Nyoni amesema Elimu ambayo wamepata wao Kama wadau wa uchaguzi ni muhimu kwenda kuifikisha Kwa wadau  wa uchaguzi hawa makundi yenye mahitaji maalum kama wazee na watu wenye ulemavu.

Imeandaliwa na Farida Mussa

Ofisi ya Habari ya Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 3,2020

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.