• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAFAHAMU mashujaa 800 waliouawa na wajerumani Litembo mkoani Ruvuma mwaka 1902

Imewekwa kuanzia tarehe: November 23rd, 2020


Jiwe la Litembo lililopo wilayani Mbinga mkoani Ruvuma,lina utajiri wa utalii wa kishujaa na kihistoria kutokana na mababu na mabibi zetu takribani 800 waliuwawa na wakoloni wa kijerumani Machi 4,1902.

Mashujaa hao waliuawa kikatili katika vita ambayo walikataa kutawaliwa na mkoloni wa kijerumani.Jiwe ambalo yalifanyika mauaji hayo ambayo yalikuwa makazi yao linaitwa Litembo kutokana na kufanana sana na kichwa cha   mnyama  tembo.

Eneo hilo lenye kichwa kinachofanana na tembo ndiyo yalikuwa makazi na maficho ya wazee wakati wa vita dhidi ya wajerumani ambapo ndani ya jiwe hilo kuna pango refu linalotokea katika Kijiji cha Maguu wilayani Mbinga.Inaelezwa ndani ya pango hilo kuna Wanyama wakali,nyoka,maji mengi,pia inadaiwa kuna madini ya zebaki na samani za chuma.

Katibu wa Baraza la Mila na Utamaduni Kata ya Litembo Bruno Tembo anasema mashujaa hao 800 baada ya kuuawa walizikwa katika makaburi ya Pamoja ya watu 25 katika Kijiji cha Litembo na kwamba ili kuwakumbuka mashujaa hao mnara wa makumbusho  umejengwa kwenye maeneo ya jiwe la Litembo na kwamba kila  mwaka Novemba 28 katika mnara huo yanafanyika maadhimisho ya kuwakumbuka wazee 800 waliopambana na wajerumani.

Kijiji cha Litembo pia kimepewa jina la jiwe hili ambalo lina pango refu ambalo mababu zetu walionusurika kwenye vita hiyo waliingia kwenye pango na kutokea upande wa pili wa jiwe hilo.

Katibu huyo wa Baraza la Mila na Utamaduni anabainisha kuwa kiongozi wa wajerumani aliyeitwa Korongo kutokana na ukatili wake alimtumia ujumbe kiongozi wa kabila la wamatengo mwaka 1902 kuwa anataka kuingia katika eneo hilo na kuwataka viongozi hao wa jadi kumuunga mkono ili kuwa chini yake.

Anasimulia zaidi  kuwa kiongozi wa wamatengo baada ya kupata ujumbe huo alipiga ngoma kubwa kwa ajili ya kuwakusanya wananchi ambao aliwaeleza kuhusu ujumbe huo wa Korongo ambapo kwa pamoja wananchi hao walikataa kuwa chini ya wakoloni wa kijerumani.

Kutokana na maamuzi hayo ya wazee Korongo  wa Kijerumani aliamua kuwapeleka wapiganaji wake wakiwa na bunduki 19 ili kupigana na mashujaa wa kabila la wamatengo.

Mababu zetu hawakuogopa walijipanga wakiwa wamejitokeza kwa mamia kwa kutumia silaha za jadi walijipanga nyuma ya jiwe la Litembo na kuanza kupambana na wakoloni wa kijerumani,hata hivyo wajerumani walitumia risasi za moto kuwauwa mashujaa  800 kikatili.

“Damu za mashujaa wa kabila la wamatengo waliouwawa na wajerumani zilichuruzika kwenye mto Mapipa ambao unaanzia kwenye milima ya Umatengo hadi kwenye ziwa Nyasa.Mashujaa walionusurika waliingia kwenye pango la jiwe la Litembo ambalo      linachukua saa nne na kutokea upande wa pili katika Kijiji cha Maguu’’,anasema Tembo.

Hata hivyo Tembo anasema kiongozi wa wajerumani baada ya kuwauwa mashujaa 800 akiwa na wenzake aliamua kuchoma nyumba zote moto pamoja na vyakula vyote viliteketezwa na kufanya uharibifu mkubwa katika eneo hilo la wamatengo.

Salvius Nyamajabeni ni Mwenyekiti Baraza la Mila na Utamaduni wa kabila la wamatengo aliyechaguliwa tangu mwaka 1958 anasema, mara baada ya mashujaa hao kuuwawa walizikwa katika makaburi ya Pamoja ambapo kila kaburi walizikwa mashujaa zaidi ya 25 kishujaa katika eneo la Litembo.

Afisa Maliasili na Utalii Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe anasema,wamedhamiria  kuvitangaza vivutio vya utalii wa kihistoria  na kishujaa vilivyopo eneo la Litembo  ili watalii wengi waweze kufika na kuona namna mababu zetu walivyoshiriki katika harakati za ukombozi dhidi ya wakoloni wa kijerumani.

Makala imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Novemba 23,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.