• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAFANYAKAZI watakiwa kuzingatia misingi ya utawala bora

Imewekwa kuanzia tarehe: May 1st, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, Mhe. Peres Magiri, amewataka watumishi kuzingatia misingi ya utawala bora ili kuondoa kero katika utumishi na kuondoa migogoro kati ya waajiri na wafanyakazi.

Ametoa wito huo wakati akisoma hotuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani, ambayo kimkoa yamefanyika katika uwanja wa Majimaji manispaa ya Songea.

"Jambo moja ambalo litatusaidia kuondoa kero katika utumishi ni kuzingatia misingi ya utawala bora, utawala bora si tu husaidia kutatua kero za wafanyakazi, pia huepusha mikwaruzano na migogoro kati ya mwajiri na mfanyakazi, na uzoefu unaonyesha kuwa migogoro ya wafanyakazi na waajiri hujitokeza ambapo kanuni za utawala bora za ushirikishwaji, uwajibikaji na uwazi hazifuatwi," alisema Mhe. Magiri.

Amebainisha kuwa Serikali inatambua kuwa wafanyakazi wamekuwa na mchango mkubwa katika kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuwaletea maendeleo wananchi.

Pamoja na mambo mengine Mhe. Magiri amewataka waajiri na wafanyakazi kushirikiana ili kuhakikisha vyanzo vinavyosababisha kero, changamoto na migogoro katika utumishi vinazuiwa ili kuleta maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla huku Serikali ya Awamu ya Sita ikiendelea kufanyia kazi changamoto za wafanyakazi na maslahi ya wanaostaafu na wanaotarajia kustaafu.

Naye Mratibu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Mkoa wa Ruvuma (TUCTA), Arab Bakari, amesema kama vyama vya wafanyakazi wanakemea vikali watumishi wasiowajibika, wabadhilifu wa mali za umma, wazembe, wanaojihusisha na vitendo vya rushwa na unywaji wa Pombe kupindukia katika maeneo ya kazi kwa kuwa ni vitendo visivyokubalika katika utumishi wowote.

Kila mwaka, tarehe 1 Mei, dunia huadhimisha Siku ya Wafanyakazi, ikiwa ni fursa ya kuwakumbuka na kuwapa heshima wale waliojitokeza kwa ujasiri kupinga manyanyaso na ukiukwaji wa haki za binadamu. Wafanyakazi hao wa awali walipambana dhidi ya unyonyaji wa mabepari katika kipindi cha Mapinduzi ya Viwanda na Kilimo mnamo Karne ya 18, wakitaka mazingira bora ya kazi na haki zao kutambuliwa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.