• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKAZI 1,138 kunufaika na mradi wa maji ya bomba Muhukuru Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: July 12th, 2020

WAKAZI 1,138 WANUFAIKA NA MRADI WA MAJI MUHUKURU SONGEA

WAKALA wa Maji na usafi wa mazingira RUWASA wilaya ya Songea mkoani Ruvuma wametekeleza mradi wa maji mtiririko wa Muhukulu kwa thamani ya sh.milioni 138 ambao utawanufaisha wakazi 1,138.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma, Meneja wa RUWASA wilaya ya Songea Mhandisi Samwel Sanya  amesema kukamilika kwa mradi huo kutawezesha kuvihudumia vijiji vya Muhukuru, Lilai,Mkayukayu na Muhukuru barabarani.

Amesema utekelezaji wa mradi huo ulianza mwaka 2014 na wafadhili kutoka Abasia ya Hanga kwa kushirikiana na wananchi wa vijiji vya Lilai na Muhukuru barabarani ambapo ujenzi wa matanki mawili ya maji yenye ujazo wa lita 50,000 na lita 75,000 ulifanyika.

Sanya amezitaja kazi nyingine zilizofanyika katika utekelezaji wa mradi huo kuwa ni kuchimba mtaro na kulaza bomba kuu la kusambaza maji umbali wa kilometa tatu,kujenga vituo 14 vya  kuchotea maji katika kijiji cha Lilahi na vituo vitatu katika kijiji cha Barabarani.

“Sisi kama RUWASA tumechimba mtaro wa kusambaza maji katika vijiji vya Lilahi na Barabarani umbali wa kilometa 24.6,ujenzi wa vituo kumi vya kuchotea maji kijiji cha Lilahi,ujenzi wa vituo 15 vya kuchotea maji na ujenzi wa chemba kwa ajili ya mita’’,alisema Mhandisi Sanya.

Hata hivyo Sanya amesema hadi sasa maji yanapatikana katika vituo 40 na kwamba RUWASA inaendelea na kazi ya kuunda jumuiya za watumia maji kwa kufuata sheria namba tano ya mwaka 2019 kwa lengo la kuhakikisha rasilimali za maji zinasimamiwa vizuri na wananchi wenyewe.

Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma ameipongeza serikali kwa kutoa fedha ambazo zimetekeleza mradi huo ambapo ametoa rai kwa wananchi kulinda miundombinu ya maji ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Naye Felista Nyoni mkazi wa Muhukuru amesema kabla ya serikali kuwapatia maji ya bomba,walikuwa wanasafiri kila siku umbali wa saa tano kwenda na kurudi kutafuta maji ambapo hivi sasa changamoto ya maji imebaki kuwa historia.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 13,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.