• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKAZI 6,000 Namtumbo kupata huduma ya maji

Imewekwa kuanzia tarehe: February 28th, 2025

Zaidi ya wakazi 6,000 wa vijiji vya Kilimasera, Ukiwayuyu, Mtakanini, Mterawamwahi, na Matependwe, wilayani Namtumbo, mkoani Ruvuma, wanatarajia kuondokana na tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama kufuatia utekelezaji wa mradi wa uchimbaji wa visima virefu vitano.

Serikali kupitia Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) imeidhinisha Shilingi milioni 300 kwa ajili ya mradi huo, ikiwa ni sehemu ya mpango wa uchimbaji wa visima 900 kwa kila jimbo nchini.

Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Namtumbo, Salome Method, amesema uchimbaji wa visima hivyo ulianza Oktoba 2024 na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Februari 2025.

“Kazi zilizopangwa ni uchimbaji wa visima, ujenzi wa vioski vya kuchotea maji, ujenzi wa mfumo wa usambazaji maji, uwekaji wa matenki ya lita 10,000 kwa kila kijiji, ufungaji wa pampu za kusukuma maji na mifumo ya umeme wa jua,” alisema Method.

Aliongeza kuwa uchimbaji wa visima na ununuzi wa vifaa muhimu umekamilika, huku ujenzi wa vioski ukiwa umefikia zaidi ya asilimia 80.

Diwani wa Kata ya Ligera, Somebody Mhongo, ameishukuru serikali kwa kufanikisha mradi huo, hasa kwa kijiji cha Mterawamwahi ambacho kwa muda mrefu kimekuwa kikitegemea maji yasiyo safi kutoka mabonde na mito.

Mtendaji wa Kijiji cha Mterawamwahi, Joseph Haule, amesema kijiji hicho kinategemea mabomba mawili ya kupampu kwa mkono ambayo hayawezi kukidhi mahitaji ya wakazi wake.

Wakazi wa eneo hilo wameeleza kuwa tatizo la maji limeleta changamoto nyingi, ikiwemo migogoro ya ndoa kutokana na wake zao kuchelewa kurudi nyumbani wakisaka maji.

Lucy Mgala, mmoja wa wakazi, amesema wanawake hulazimika kwenda kuchota maji mtoni na mabondeni, jambo linalowakabili na hatari mbalimbali, hususan msimu wa masika.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru 2025 waikubali miradi yote Mbinga

    May 12, 2025
  • WANANCHI walivyojitokeza kuupokea mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Maguu Mbinga

    May 11, 2025
  • MAHABA ya wananchi wa Mbuji wilayani Mbinga kwa Mwenge wa Uhuru 2025

    May 11, 2025
  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.