• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA Ruvuma wanavyonufaika na mfumo wa stakabadhi ghalani

Imewekwa kuanzia tarehe: September 27th, 2021

WAKULIMA Ruvuma wamenufaika na mfumo wa Mazao Stakabadhi  Ghalani kwa misimu mitatu  mfululizo kwa mazao ya Ufuta,Mbaazi,Soya, Korosho na Kahawa kwa zaidi ya Shilingi bilioni 283.

Akitoa taarifa hiyo Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Jeremia Sendoro amesema uendeshaji wa mazao ya Ufuta,Soya pamoja na Mbaazi umefanyika kupitia wakulima kukusanya mazao kupitia vyama vya msingi 88 na vyama vikuu .

Amesema kwa msimu wa mwaka 2020/2021 jumla ya minada 29 ya ufuta ilifanyika ambapo jumla kilo 8,326,686 za ufuta ziliuzwa kwa bei ya juu sh.2,393 na bei ya chini 1,998 na kuwapatia wakulima zaidi ya shilingi milioni 17,na kwa kipindi cha msimu wa mwaka 2018/2019 hadi 2021 Julai Mkoa wa Ruvuma ulukusanya kilo za ufuta 28,989,711 na kuuza kwa bei ya sh2,393 wakulima walipata zaidi ya shilingi bilioni 69.

Hata hivyo Sendoro amesema kwa msimu wa kilimo cha 2018/2019 hadi 2021 Julai jumla ya kilo za Soya zilikusanywa kwa wastani wa kilo 4,963,088 wakulima walijipatia kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 5.

Amesema kwa zao la Mbaazi mwaka 2018/2019 hadi 2021 Septemba walikusanya wastani wa kilo 12,165,680 wakulima walijipatia zaidi ya shilingi bilioni 12,Korosho mwaka 2017/2018 hadi kufikia mwaka 2020/2021 walikusanya kilo 79,535,246 na wakulima walipata zaidi ya shilingi bilioni 241 pamoja na zao la Kahawa mwaka 2017/2018 hadi kufikia msimu wa mwaka 2020/2021 jumla ya kilo 63,908,344  kahawa zilikusanywa na kuuzwa kwa bei 4,000  wakulima walijipatia zaidi ya shilingi bilioni 255.

Akizungumzia mafanikio ya mfumo wa stakabadhi ghalaniSendoro amesema ikiwemo wakulima kupata bei nzuri hususani mzao yanayouzwa katika mfumo huo,kuwepo kwa ushirikiano mzuri kwa wadau,kuwepo kwa matumizi sahihi ya vipimo,kupunguza kiasi cha utoroshwaji,pamoja na mapato ya Halmashauri.

Katibu tawala msaidizi amesema changamoto za mfumo huo baadhi ya madalali  kuwashawishi na kuwarubuni wakulima,Uelewa wa mfumo huo bado upo chini hususani Halmashauri ya Madaba na Nyasa upo chini,Hali ya mazao bado upo chini kitija pamoja na kuto pima hali ya afya ya udongo.

Sendoro ameeleza mpango mkakati wa kukabiliana na changamoto hizo kuwa Mkoa wa Ruvuma umejipanga kusimamia mfumo wa stakabadhi ghalani kwa kuwa umeleta auheni kwa wakulima,Mkoa umeendelea kusimamia maelekezo ya Serikali Maafisa ugani waelekeze majukumu yao na wasimamie ipasavyo.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amesema kapitia mfumo wa stakabadhi ghalani siyo kuboresha mfumo bali kuanzia mbegu bora  ili Mkoa wa Ruvuma uwe na kilimo cha tija zaidi na uwezo wa kuandaa mashamba kabla ya kulima .

“Tumejipanga kuanza kilimo cha mazao ya biashara kikubwa zaidi cha kimkakati ikiwemo grobal farming kinavyoelekeza hata ilani ya CCM inaelekeza”.

Hata hivyo Ibuge amekaribisha kilimo cha mkataba katika Mkoa huo na kitakuwa cha bei nzuri  wakati wa mavuno ni fursa kwa wakulima na kuendelea kuimarisha Ushirika.

Amesema mfumo wa  stakabadhi ghalani unamhakikishi mkulima usalama katika kuuzao mazao yake na amewasihi viongozi wanaosimamia  vyama vya msingi kuwa wazalendo nakuto wapunja wakulima ili waendelee kunufaika na mfumo huo.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma

Septemba 27,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.