• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA Tunduru wauza tani 824 za mbaazi kupitia stakabadhi ghalani

Imewekwa kuanzia tarehe: August 14th, 2023

TANI 824 sawa na kilo 824,941 zenye thamani ya Sh.bilioni 1,663,081,056 za zao  la mbaazi zimenunuliwa kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani katika mnada wa kwanza wa zao hilo uliofanyika katika kijiji cha Majimaji wilayani Tunduru.

Katika mnada huo makampuni ishirini yalijitokeza kuomba kununua mbaazi za wakulima,hata hivyo ni makampuni matatu ndiyo yaliyofanikiwa kununua  mbaazi zote zilizokusanywa na chama cha msingi cha Majimaji  kutoka kwa wakulima kwa bei ya Sh.2,016 kwa kilo moja.

Akizungumza na wakulima Mwenyekiti wa Chama kikuu cha Ushirika wilaya ya Tunduru(TAMCU ) Ltd)Mussa Manjaule amewapongeza wakulima wa kijiji hicho kwa uzalishaji mkubwa na kukubali kuuza mbaazi zao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.

Alisema,msimu uliopita bei ya mbaazi  katika mnada wa kwanza  bei ya chini ilikuwa Sh.850 na bei ya juu Sh.950 na hata katika mnada wa mwisho bei ilikuwa Sh.1,020 tofauti na mwaka huu  ambapo bei katika mnada wa kwanza ni Sh.2,016.

Alisema,zao la mbaazi limeendelea kufanya vizuri kutokana na kununuliwa kwa bei kubwa na hivyo kuwa miongoni mwa mazao yanayowaingia wakulima fedha nyingi katika wilaya ya Tunduru.

Hata hivyo,amewataka wakulima kuongeza uzalishaji kwa kupanua mashamba yao na kulima mazao  mbalimbali ikiwemo ufuta,korosho na mbaazi ili waweze kupata fedha nyingi na kuondokana na umaskini kupitia shughuli zao za kilimo.

Meneja wa Chama kikuu cha Ushirika(TAMCU Ltd) Imani Kalembo, amewaomba wanunuzi kuongeza bei ya kununua mbaazi  ili kuwahamasisha wakulima kuzalisha kwa wingi mbaazi na mazao mengine ya biashara  yanayostawi vizuri  katika maeneo mbalimbali wilayani humo.

“wanunuzi wakiongeza bei,wakulima wanapata moyo wa kuongeza uzalishaji na kuamini kuwa serikali iko pamoja na wao kwa kusimamia suala la bei ya mazao yao yanayouzwa kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani”alisema Kalembo.

Amewaomba wakulima kuwa na utaratibu wa kujitokeza kwa wingi kwenye minada inayofanyika katika maeneo yao, kwani lengo la Chama kikuu ni kuhakikisha minada yote inafanyika kwa uwazi ili wakulima wafahamu bei zinazotolewa na wanunuzi.

Kwa upande wake Afisa ushirika wa wilaya ya Tunduru George Bissan  alisema,wakulima wa wilaya hiyo wana bahati kubwa kwa kupata soko la uhakika na bei nzuri ya mazao  wanayozalisha.

Bissan amewataka wakulima kuwa na uvumilivu baada ya mavuno ili kuuza mazao kupitia vyama vyao vya msingi vya ushirika kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani wenye faida kubwa na kukataa kuuza kwa walanguzi kwa bei ndogo isiyolingana na gharama za uzalishaji.

Amewaonya viongozi wa vyama vya msingi(Amcos),kuepuka udanganyifu  badala yake kuwa waaminifu na waadilifu kwa kulipa fedha za wakulima  kwa wakati ili kusitokee malalamiko na kushusha hali ya uzalishaji mashambani.

Katika hatua nyingine Bissan,amewahimiza vijana wilayani humo kujikita katika shughuli za kilimo badala ya kutumia muda  mwingi vijiweni kucheza pool na bao,tabia inayo warudisha nyuma na kukithiri kwa umaskini miongoni mwao.

Mwakilishi wa wakulima wa mbaazi Seif Kaunda,ameishukuru serikali kwa kusimamia ununuzi wa zao la mbaazi kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani kwani umewasaidia kupata soko la uhakika na bei nzuri ambayo inakwenda kuboresha maisha yao na kuhamasisha watu wengi kujikita kwenye k

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.