• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA wa korosho Kusini waomba pembejeo

Imewekwa kuanzia tarehe: July 23rd, 2022

Wakulima wa korosho mikoa ya Ruvuma ,Lindi na Mtwara wameiomba serikali kuwapelekea pembejeo za korosho za kutosha na kwa wakati ili kuongeza uzalishaji wa zao la korosho ambalo linauzwa kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani.

Wakulima hao kutoka Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma ,Wilaya ya Nanyumbu mkoani Mtwara na Wilaya ya Lindi mkoani Lindi wametoa maombi hayo walipotembelewa kwa nyakati tofauti na Mkurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa stakabadhi ghalani nchini Asangye Bangu.

Khalid Machemba Mkulima wa Namatili Wilaya ya Tunduru amesema kuuza korosho kupitia stakabadhi ghalani ni jambo nzuri isipokuwa changamoto kubwa inayowakabili hivi sasa ni upungufu wa pembejeo za korosho ambazo hazitoshelezi mahitaji ya wakulima hali ambayo amesema inaweza kuchangia kushusha uzalishaji wa zao hilo.

Ally Athuman Mkulima wa Nanyumbu mkoani Mtwara amesema licha ya ukweli kwamba zao la korosho ni dhahabu ya kijani wakulima wanakabiliwa na upungufu wa dawa za kupulizia kwenye mikorosho hali ambayo amesema inayoweza kuathiri zao hilo.

Ally pia ameomba bei ya korosho iongezeke kwa sababu hivi sasa imeshuka na kuathiri wakulima.

Mohamed Juma Mkulima wa Nachunyu Mtama Halmashauri ya Lindi  amesema pembejeo za korosho walizopewa msimu huu hazikidhi mahitaji ya wakulima ambao ni wengi na wana mashamba makubwa.

Musa Nura Mkulima wa kijiji cha Malungo Wilaya ya Lindi amesema kijiji chenye wakulima wa korosho 500 kupewa mgawo wa mifuko 100 ya viuatilifu inaleta changamoto kubwa kwa wagawaji hivyo ameiomba serikali kuongeza mgao wa pembejeo ili kuwa na uhakika wa kuongeza uzalishaji wa korosho

Akijibu maombi hayo Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Bodi ya Korosho Tanzania Enock Ngalaba amesema serikali inalitegemea zao la korosho kwa ajili ya kukuza uchumi wa wakulima na serikali kwa ujumla hivyo serikali itayafanyia kazi maombi hayo ya wakulima wa zao la korosho ili dawa ziwafikie wakulima kwa wakati.

"Ndiyo maana hata Mkurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa stakabadhi ghalani nchini ameamua kufanya ziara ya kuwatembelea ili kuonana uso kwa uso na wakulima  wenyewe na kusikiliza kero zinazowakabili",alisema

Amesisitiza kuwa serikali ni sikivu na itachukua hatua haraka kwa sababu uzalishaji wa zao la korosho ukipungua na serikali inapunguza mapato yake na hivyo kurudisha nyuma maendeleo yake.

Mkurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa stakabadhi ghalani nchini Asangye Bangu akizungumzia changamoto ya pembejeo za korosho kwa wakulima wa kusini,amesema kilio cha wengi ni uwepo wa dawa kidogo za kupulizia korosho ambazo hazilingani na mahitaji ya wakulima.

"Wakulima Mimi nimewaelewa kabisa na nawaahidi kuwa nit azungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania ili kutatua kero hii kwa wakati"'alisisitiza.

Hata hivyo amesema ana taarifa kuwa serikali ilileta awamu ya kwanza ya dawa hizo na kwamba awamu ya pili pia italetwa ili kuwafikia wakulima.

Ameitaja nia ya serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha kuwa kila Mkulima anapata pembejeo za korosho kwa wakati na zinazotosheleza mahitaji ya wakulima ili kuongeza uzalishaji wa zao la korosho ambalo ni dhahabu ya kijani.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Julai 20,2022



Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.